burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

28 Des 2016

Rose Muhando akanusha kutumia Madawa ya kulevya ‘situmii madawa na sitatumia’

Msanii mkongwe wa nyimbo za Injili nchini Rose Muhando amekanusha taarifa ambazo zilizagaa katika mitandao ya kijamii kuwa ameingia katika matumizi ya Madawa ya kulevya.

Muimbaji huyo alidai taarifa hizo zilisambazwa na watu ambao hawamtakii mema katika maisha yake kutokana na kwenda nao tofauti katika makubaliano ya kufanya nao kazi.

“Situmii madawa na sitatumia, kama waliona ndiyo skendo itakayonimaliza wameshindwa, wanaofanya hivyo ni watu wanaotaka kunimaliza walitaka nifanye kazi zao, nikakataa.” Rose aliuambiia mtandao wa gazeti la Mwanaspoti.

Aliongeza, “Sijajiingiza na mambo hayo na wanavyozungumza nasikitika kwa sababu wanaiumiza familia yangu kisaikolojia, mimi ni mama wa watoto watatu na nina ndugu zangu, naambiwa mambo yote hayo kwa sababu sina mtu wa kunitetea,”

Katika katua nyingine muimbaji huyo alizungumzia kuhusu ukimya wake pamoja na ujio wake mpya.

“Nipo hata hivyo kuna kazi nyingine nimeandaa ipo kwa Alex Msama bado haijatoka kutokana na mambo mbalimbali, ingawa naandaa kazi nyingine ninayotegemea kuikamilisha mwezi wa tatu mwakani tutakapojaaliwa. Nimeshaanza kuandaa baadhi ya nyimbo na nyingine naendelea kutunga, unajua kazi hizi huwa nasikiliza sauti ya Mungu aniambie niimbe nini.”

“Pia, nimekuwa nafanya huduma ya kuimba katika mikutano tofauti ndani na nje ya nchi kama hivi jana umenikuta natoka kijiji cha jirani kuimba na wiki iliyopita, nilikuwa Kenya ambako nilifanya huduma, Kisumu na Mombasa, nimeamua kufanya hivyo kwa sababu zangu,” anasema Rose.

27 Des 2016

happy birthday boss wa blog ya g.lovetz

Picha ya Godlov Kilave
Image result for happy birthday
leo ni siku ya kuzaliwa boss wa blog ya g.lovetz amepanga mambo ya maendeleo katika mwaka ujao pia katika blog yake amejipanga vilivyo g.lovetz ni mmoja kati ya wasanii wachanga wanaofanya vizr katika mzik wa bongo fleva

Madee aumizwa na picha za Chid Benz mtandaoni


Madee ameonyesha kukerwa na kitendo cha baadhi ya watu kumpiga picha Chid Benz na kuzisambaza mtandaoni.

Hitmaker wa Migulu Pande kupitia mtandao wa Twitter ametoa yake ya moyoni kwa kusema kuwa kitendo cha kumpiga picha rapper huyo na kumuanika mitandani ni kumdhalilisha.

“Hawa wanaompigapiga picha @ChidiBeenz na kupost kwenye mitandao yao lengo lao kubwa ni nini?mbona tunazid kumdhalilisha?au mnataka kiki?,” ameandika Madee.

Kuna uwezekanao mkubwa kauli hiyo ya Madee imekuja baada ya kuona kipandwe cha video alichopost Solo Thang kwenye mtandao wake wa Instagram akiwa na Chid Benz huku afya yake ikionekana kuzidi kuwa mbaya.

Ben wa bongo movie apata ajali mbaya ya gari, alazwa Muhimbili


Msanii mkongwe wa filamu za vichekesho,  Ben Branco Selengo amelazwa katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili baada ya kupata ajali mbaya ya gari siku ya sikukuu ya Christmas.

Muigizaji Mboto ambaye ni rafiki wa karibu wa Ben, kupitia instagram ameandika:

Ajali ulioipata sio ndogo kwetu sisi wanadam, lakin kwa mungu ni ndooogo sana. Naamin ndogo kwa mungu kwasababu utapona kwa uwezo wake mungu. Utapona tu inshaallah (Benn Blanco Selengo)

Akiongea na Bongo5 asubuhi hii ndugu wa karibu wa Ben kupitia simu ya Ben, alidai Ben alipata ajali mbaya ya gari juzi na hali yake bado ni mbaya.

“Ben hali yake siyo nzuri kusema kweli,” alisema dada huyo aliyejitambulisha kwa jina na Sarah. “Alipata ajali ya gari juzi na hapa tunapozungumza bado yupo Muhimbili hospitali.”

Hali ya Chidi Benz yamshtua Solo Thang

Msanii mkongwe wa muziki wa hip hop, Solo Thang ameposti video akiwa na rapa Chidi Benz ambaye walikutana usiku na kuongea baadhi ya mambo, lakini kutokana na hali aliyokuwa nayo Chidi Benz Solo Thang alisema hawezi kumuhukumu bali anastahili kuombewa tu.

Katika ujumbe ambao Solo Thang aliandika kwenye mtandao wake wa Instgram alisema hawezi kuhukumu na hata iweje bado Chidi Benz ataendelea kuwa mdogo wake, rafiki yake na mtu wake wa karibu.

“Met with my Young brother Chid Benz last night almost cried, I dont judge, no matter what still my hommie, tumeongea sana, tuzidi kumuombea Mola” aliandika Solo Thang

Utampenda Ray C akiwa ndani ya muonekano mpya wa kihindi

Huwenda huu ukawa ndio ujio mpya wa msanii mkongwe wa muziki wa bongofleva Rehema Chalamika aka Ray C baada ya misukosuko ya hapa na pale katika maisha yake ya muziki.

Muimbaji huyo ambaye amedaiwa kuweza kuachana na matumizi ya Madawa ya kulevya baada ya kushindwa kwa muda mrefu,wiki chache zilizopita aliweka kambi ndani ya studio ya Wanene kwa ajili ya maandalizi ya ujio wake mpya.

wiki hii amepiga picha zake mpya zinazomuonyesha akiwa na muonekano wa kihindi.

Nahreel ni miongoni mwa maproducer watakaonibadilisha – Chemical


Chemical amefunguka jinsi alivyojisikia baada ya kufanya kazi na Nahreel.
Mashabiki wamezoea kumuona Chemical akiachia kazi zake ambaozo zimetayarishwa na Maximizer lakini kwenye project mpya ya ‘Hola Hola’ imekuwa ya kwanza kumsikia rapper huyo akifanya na producer mwingine.

Akiongea na g.lovetz, Chemical amesema, “Nilifurahi kufanya kazi na Nahreel kwa sababu ni mtu ambaye nilikuwa natamani kufanya naye ngoma, ukiachana na hiyo ‘Hola Hola’ nilikuwa natamani sana kufanya naye ngoma yangu kama mimi.”

“Baada ya hiyo ‘ hola Hola’ nahisi kuna project yoyote nyingine inaweza ikatokea nikafanya na Nahreel na nitashukuru na nitapenda sana kwa sababu nahisi atakuwa ni miongoni mwa maproducer watakaweza kumbadilisha Chemical watu wakasikia ladha nyingine,” ameongeza.

Mapenzi yangu na Jacqueline Wolper yapo moyoni – Harmonize


Msanii wa muziki kutoka WCB, Harmonize amekanusha kuachana na mpenzi wake Jacqueline Wolper baada ya hivi karibuni kuzagaa taarifa katika mitandao ya kijamii kuwa wawili hao wameachana.

Madai hayo yalichukua sura mpya wiki chache zilizopita baada ya malkia huyo wa filamu kudaiwa kufuta picha za mkali huo wa wimbo Bado katika mtandao wake wa instagram.

Akiongea jana katika kipindi cha XXL cha Clouds FM, Harmonize alidai mapenzi yao yapo moyoni na watu wasichanganywe na issue ya kufuta picha instagram.

“Wolper alifuta tu picha za instagram hakufuta mapenzi yetu yapo moyoni,” alisema Harmonize.

Pia muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo Matatizo, alidai suala la malkia huyo kufuta picha instagram ni kawaida kwani anaweza kufuta na kuanza kupost mpya.

Wapenzi hao wamebadili utaratibu wa maisha yao kwani huko nyuma walikuwa wanasafiri na kula bata pamoja.

Kwa sasa WCB tunadeal na label za wasanii hatuwezi kusaini wasanii wote – Sallam


Meneja wa Diamond Platnumz, Sallam aka Mendez amedai label ya WCB inaandaa mkakati wa kudeal na label mbalimbali za wasanii na sio kuendelea kusaini msanii mmoja mmoja.

Akijibu swali la mmoja kati ya mashabiki ambao walijitokeza jana Mlimani City ambalo lilihoji label ya WCB imejipanga vipi kuendelea kusaini wasanii wapya, Sallam alidai wao kama WCB watakuwa wanadeal na label na sio msanii mmoja mmoja.

“Kwa sasa tunasaini na label,” alisema Sallam. “Kwa hiyo label ambayo utakuwa wewe itakuwa chini ya WCB na WCB kazi zako tutazipeleka mbali kabisa,”.

Aliongeza,”Tukiwachukua wasanii wote WCB peke yake, tutakuwa wachoyo na sisi hatutaki kuwa wachoyo. Kwa hiyo label nyingi zifunguke na WCB tutadeal na label hatuwezi kudeal na msanii mmoja mmoja kwa sababu nauhakika milioni 10 ya watanzania ni wasanii,”

Kwa sasa label ya WCB ina miliki wasanii wanne, Rich Mavoko, Rayvanny, Harmonize pamoja na Queen Daren.

Official VIDEO | Masanja Ft. Walter - MONICA | Watch


24 Des 2016

Uongozi mzima wa G.LOVETZ BLOGSPOT unakutakia heri ya X-MAS NA MWAKA MPYA

Image result for X-MAS
BOSS wa blog ya g.lovetz anawatakia heri ya x-mas na mwaka mpya pia amesema mwakani ni mwaka wa mapinduzi katika blog hii mambo ya kisasa utayakuta pia utaratibu utaboreshwa zaidi kuwa wa kisasa inakualika kuangalia kila page 
mambo mengi na mzuri pia yataongezwa katika mwaka ujao
maoni yako ni muhimu kwetu ili kuboresha huduma zetu katika utoaji wa habari mpya pamoja na nyimbo mpya

pia waweza kutupata katika mitandao mingine gusa HAPA kupata kila kinachojili 

MERRY X-MAS
&
HAPPY NEW YEAR

Mjini hakuna kulima twende zetu mkoa pata shamba heka 4 M 6.5 lipo mafinga kijiji cha nyororo

Image result for mashamba

pata shamba lenye ukubwa wa hekari 4 kwa million 6 na nusu 
shamba lipo mafinga mkoani iringa katika kijiji cha nyororo 
wasiliana nasi 
kwa 
+255 715 952 025

Official VIDEO | Killy – Nikwambie | Watch

Image result for Killy – Nikwambie


Papa Misifa adai hatamsahau Rich Mavoko mpaka anaingia kaburini!

Image result for richi mavoko
Aliyewahi kuwa meneja wa zamani wa Rich Mavoko, Papa Misifa amefuguka kwa kudai kuwa Rich Mavoko ni msanii ambaye hatakuja kumsahau mpaka anaingia karibuni kutokana na mambo aliyotendewa na msanii huyo.

Mkurugenzi huyo wa label ya Al Jazeera Entertainment ambayo inamsimamia, Killy, Aly Nipishe pamoja na Rhymes Biashara, amedai mpaka leo bado anamdai Rich Mavoko na kesi ipo Mahakamani.

“Mimi katika wasanii ambao sitawasahau katika maisha yangu ni Rich Mavoko, yule mtoto hana adabu,” Papa Misifa alikiambia kipindi cha FNL cha EATV. “Mpaka kesho bado namdai na kesi ipo mahakamani. Yule tulipanga kwenda kushoot video Afrika Kusini, sasa kuna hela alikuwa nayo yeye akaondoka nayo,”

Pia Papa alidai muimbaji huyo hawezi kufanikiwa zaidi kwa kuwa tayari kuna mambo mabaya nyumba aliyafanya na anatakiwa kuyarekebisha pamoja na kuomba msamaha.

Kwa sasa Rich Mavoko yupo katika label ya WCB ya Diamond na anafanya vizuri na wimbo wake mpya, Kokoro.

Salome na Pana zaongoza orodha ya nyimbo kubwa 10 za mwaka kwa mujibu wa tovuti ya The Gurdian ya UK


Gazeti maarufu la Uingereza, The Guardian kupitia tovuti yake, limetoa orodha ya nyimbo 10 zilizokuwa kubwa Afrika mwaka 2016. Kwenye orodha hiyo, Diamond na Alikiba wamo. Pana ya Tekno wa Nigeria imeshika nafasi ya kwanza na kufuatiwa na Salome ya Diamond na Ray Vanny.

“In the 90s, Tanzanian legend Saida Karoli’s classic Maria Salome was a hit across most of east Africa and was one of the soundtracks to Tyler Perry’s 2013 film, Peeples,” wameandika.

“More than two decades later, a remake by her compatriot Naseeb Abdul Juma – better known in these parts as the singing sensation Diamond Platnumz – has become a hit, too. The 27-year-old’s version features Wasafi Music labelmate Rayvanny and combines some of the best traditional outfits across Africa in its colourful slideshow of a video that has over 10m YouTube views. It’s a Kiswahili extravaganza.”

Kwenye collabo ya Sauti Sol na Alikiba, Unconditionally Bae wameandika: After clinching a nomination for best international act at the BET awards and getting Barack Obama to do the Lipala dance in 2015, frontline Kenyan boy band Sauti Sol’s hot streak continued this year with the stellar monochrome visuals for the a cappella hit Kuliko Jana. Their biggest work was linking with Tanzania’s Alikiba (who signed to Sony Music this year) for the dance number Unconditionally Bae, which has racked up over 4m YouTube views.”

Hii ni orodha nzima:

Tekno – Pana
Diamond Platnumz feat Rayvanny – Salome
Mr Eazi feat Joey B and Dammy Krane – Hollup
Patoranking feat Sarkodie – No Kissing Baby
Babe Wodumo feat Mampintsha – Wololo
Eugy x Mr Eazi – Dance for Me
Kwesta feat Cassper Nyovest – Ngudu
Yemi Alade – Koffi Anan
DJ Maphorisa feat Wizkid, DJ Buckz – Soweto Baby
Sauti Sol and Alikiba – Unconditionally Bae

Official VIDEO | Lameck Ditto - Moyo Sukuma Damu | Watch


Kuanzia 2017 Ben Pol adai atatoza shilingi milioni 10 kwa collabo

Unataka kufanya collabo na Ben Pol? Muwahi sasa kabla ya Disemba 31, sababu mwaka 2017, mambo yanakwenda kubadilika.

Ben Pol amesema kuanzia mwakani atakuwa akitoa dola 5,000 kwa kila kolabo ambayo ni zaidi ya shilingi milioni 10 za Kitanzania.

“Kuelekea 2017 bei yangu ya Collabo itakuwa $5000. So kama una project na mimi tuwasiliane before 31st Dec 2016,” aliandika Ben kwenye Twitter.

“Ni kweli, ila kama wimbo ni mkali tunaweza kukaa mezani na huyo mtu akanipa sehemu ya umiliki wa hiyo kazi,” Ben ameiambia Bongo5 baada ya kumuuliza kama amedhamiria kweli.

“Kwanza nataka kupunguza idadi ya colabo ili nifanye chache za walio serious na wanaoweza kupush hizo project. Mfano mtu hawezi kukulipa dola elfu 5 halafu akaiweka ngoma kwenye album, au akaiweka ndani tu,” amesisitiza.

“Pia itasaidia kwangu kufikiria zaidi kwenye hiyo kazi, hakuna mtu atakulipa dola 5 halafu akatarajia disappointment, so ita-benefit kwa pande zote.”

‘Hola Hola’ haijaharibu mipango yangu – Chemical


Rapper wa kike Bongo mwenye mistari na swaga za hatari, Chemical amedai kuwa project ya ‘Hola Hola’ haijaharibu mipango yake ya kufanya collabo na rapper mwingine wa kike.

Chemical ameiambia g.lovetz kuwa project hiyo haijaathiri chochote juu ya mipango yake hiyo ila ataangalia kama kuna rapper mzuri atakaye fit kwenye kazi yake atamshirikisha.

“Kukiwa na project yangu yoyote ambayo nitahisi kuna female rapper anatakiwa awepo nitafanya hivyo haimaanishi kuwa Hola Hola ndio imebadilisha mipango yangu wala nini. Lakini kazi yenyewe itabidi tuangalie kama kuna mtu atafiti kwenye kazi yangu nitafanya naye,” amesema Chemical.

Kwa sasa Rapper huyo anafanya vizuri kwenye vituo mbalimbali vya redio na runinga kupitia wimbo wake ‘Mary Mary’.

Barnaba atamani mtoto wa kike


Barnaba anatamani kupata mtoto wa kike baada ya kuwa na mtoto wa kiume, Steve.

Muimbaji huyo na mtayarishaji wa muziki ameandika kupitia mtandao wake wa Instagram kuwa moja ya ndoto zake za mwakani ni kumuomba Mungu amsaidie apate mtoto wa kike.

Kupitia mtandao huo, Hitmaker huyo wa Lover Boy ameandika:

👨‍👧ndoto Yangu nyingine Mwakani kupatamtoto wa kike Mungu akijalia Kwa uwezo wake but 🎧 #goodmusic Kwanza GoodSound Classic ⛪️Jesus is My song

23 Des 2016

Collabo na msanii wa nje isipofanya vizuri kimataifa ni kazi bure – Fid Q


Rapper Fid Q amesema msanii anapofanya collabo na msanii wa nje na wimbo huo usifanye vizuri kimataifa, ni sawa na kazi bure.

Amesema pia kuwa mafanikio ni pale unapofanya wimbo unaoweza kufika nje wenyewe kama ambavyo nyimbo za nje zinazofanya vizuri hapa nchini.

“Halafu kitu ambacho nawaambia wasanii kila siku, kila mtu anaweza akatengeneza hit lakini lakini tunatengeneza muziki unaoweza ukatrascend?” rapper huyo alisema kwenye mahojiano na mtangazaji wa Uhuru FM, Crispin Mgenge.

“Ninaposema kutrascend namaanisha kwamba ninaweza nikaenda nikawarusha Amsterdam kama ninavyowarusha Mwanza, au tu ninang’aa Mwanza halafu Amsterdam hawanielewi ninafanya nini,” amesisitiza.

“Kwahiyo kutrascend ndio kitu ninachowasisitiza wasanii wajifunze hicho, wasikimbilie tu kufanya ngoma na nani hazisaidii.”

Jay Moe anavyokula sahani moja na kizazi cha ‘dab’


Juma ‘Jay Moe’ Mchopanga aka Mbakiaji, ni rapper mkongwe ambaye kama ng’ombe mzee, hazeeki maini. Kwa takriban miaka 15 ya career yake, Jay Moe hajawahi kuonekana kuhangaika kuonesha ujuzi wake kwenye hip hop.

Ni miongoni mwa wasanii wa zamani wenye hits nyingi ambazo licha ya kuwa na muda mrefu tangu zitoke, bado zinaweza kusikika na upya masikioni mwako. Nyimbo kama Bishoo, Mvua na Jua, Kama Unataka Demu, Maisha ya Boarding, Story 3, Famous ni miongoni mwa nyimbo zake classic zilizompa heshima. Huwezi kusahau hits zingine alizoshirikishwa kama Zeze ya TID, Kimya Kimya aliyofanya na marehemu Ngwair au Jirushe ya Ferooz.

Pamoja na ukongwe huo, Jay Moe amethibitisha mwaka huu kuwa anaweza kuwa rapper hatari katika kizazi cha trap na dab. Aliamua kuchukua risk iliyozaa matunda, kufanya muziki ambao rappers wenye heshima kama yeye wanaogopa kuufanya kwa kile wanachoamini wataonekana wanatapatapa. Wimbo wake Pesa ya Madafu ulimhamisha kutoka kwenye rap yake iliyozoeleka, hadi katika rap ya vijana wa leo, rap ya kizazi cha dab.



Jay Moe anasema aliamua kubadilika kiasi hicho kutokana na kukosolewa na watu kadhaa kwenye wimbo kabla ya huo, Hili Game ambao anasema alifanya makusudi kwa kuogopa kuja na ladha mpya kufuatia ukimya wake wa muda mrefu.
Anasema hiyo ilimpa sababu ya kuja na wimbo wenye usasa mwingi kwakuwa ni nyimbo ambazo anasikiliza pia. “Huko nyuma sikuwa na wimbo ambao ungeweza kuconnect watu wa jinsia tofauti na umri tofauti,” rapper huyo alikiambia kipindi cha Ngaz Kwa Ngaz cha Salama Jabir miezi kadhaa iliyopita.

“Kwasababu umekuwa ni wimbo ambao hata watoto wadogo nikipita tu wanaimba ‘pesa ya madafu.’

Na kiukweli kubadilika kwa Jay Moe kumekuwa na mafanikio makubwa kwasababu Pesa ya Madafu haikosi kwenye orodha ya nyimbo 10 za hip hop zilizotamba zaidi kwenye redio na TV mwaka huu.

Kubadilika kwake pia, kulikuwa na sababu za kiuchumi na kugoma kuendelea kushikilia misingi ya hip hop ambayo haina faida.

“Leo wakitajwa wasanii wakali wa hip hop hata watano Jay Moe atatajwa lakini wakitajwa wasanii watano wa hip hop wenye mafanikio Jay Moe hayupo,” alisema kwenye interview moja.

“Kwanini na mimi nisiwe kama Nay wa Mitego, kwanini mimi nisiwe kama AY na Profesa Jay wakati kipaji changu kinafaa niwe hivyo, zaidi ya hivyo. Wasanii wengi wa hip hop wanataka ku-maintain culture ambayo haipo tena. Wote tunakubali kuwa sasa hivi muziki biashara kwahiyo tukubali kufanya ule wa kibiashara ambao hatutokuwa na malalamiko ‘wasanii wa zamani tunabaniwa kwenye media’ sio kweli ni kwasababu hatujapeleka content ambayo media na wasikilizaji wanaitaka,” alisisitiza rapper huyo.

Jay Moe hajaishia kwenye Pesa ya Madafu, bali amekuja kuonesha kuwa amekimudu vizuri kizazi cha trap na dab kwenye wimbo alioshirikishwa na Songa – rapper mwingine aliyeamua kubadilisha muelekeo.
Mwendo Tu, ni wimbo mwingine wa trap ambao kutokana na ulivyo, umewaongezea wigo wa mashabiki hasa ‘teenagers’ na wasichana ambao haikuwa rahisi kuwapata kwa nyimbo walizokuwa wamezoea kufanya.

Nguvu ya wimbo huo imeongezeka zaidi kutokana na kuwa na video kali inayovutia macho ya kila mpenda vitu vizuri. Kwa mabadiliko hayo ya Jay Moe, ni wazi kuwa ana miaka mingi kwenye game na rappers wengi wapya watakuja na kuondoka na kumwacha akipeta kama na wao watashindwa kuwa vinyonga.

Vanessa Mdee adai ataachia wimbo wake na Barnaba mwakani


Vanessa Mdee amethibitisha kufanya wimbo mwingine na Barnaba ambao utatoka mwakani.
Hitmaker huyo wa Cash Madame ambaye aliwahi kufanya wimbo wa ‘Siri’ na msanii huyo ambao ulitoka mwaka jana amesema kupitia mtandao wa Instagram kuwa wimbo huo ni moto hatari.

Kupitia mtandao huo, Vanessa ameandika:

GENIUS @barnabaclassic mkisikia kitu tumewa andalia kwa ajili ya 2017 uwiii MoTO MOTO MOTO @barnabaclassic




Trey Songz sio role model wangu – Jux


Jux anataka watu waelewe kitu hiki ‘once and for all’, Trey Songz sio role model wake.
Amedai kuwa kitendo cha kujichora tattoo kifuani inayofanana na msanii huyo wa Marekani, hakimaanishi kuwa ni mtu anayemuangalia kwa jicho la ‘role model.’

“Trey ni mtu ambaye napenda tu kazi zake, sio role model wangu,” alisema muimbaji huyo wa Juu kwenye mahojiano na kipindi cha The Base cha ITV.
Kuhusu kilichotokea miezi kadhaa iliyopita kati ya Vanessa Mdee na Trey walipokutana Nairobi kwenye Coke Studio ambapo picha zao zilisababisha headlines nyingi, Jux anasema alikuwa anajua kila kinachoendelea.


“Niliona picha kabla hawajaona watu wote, kwahiyo nilikuwa najua kinachoendelea, kila kitu nilikuwa nakijua,” alisema.

“Mimi ni mtu ambaye naongea na Vanessa kuliko.. naweza kusema katika watu wanaongea mara nyingi na Vanessa mimi nipo, so updates nyingi sana huwa nazipata kabla ya watu wengine. Kwahiyo hakikunishtua kile kitu. Ila watu kuanza kuongea, natamani ningeweza kusema kitu fulani na kimfikie kila mtu na ajue kinachoendelea,” amesisitiza.

Hivi karibuni wawili hao wameachia video ya wimbo wao wa pamoja, Juu.



Izzo Bizness na Abela (The Amazing) wafunguka iwapo ni wapenzi

Image result for Izzo Bizness na Abela
“Mimi na Abela ukiachana na kundi ni washkaji sana,” Izzo ameiambia Bongo5.

“Unajua sababu hata nitakuja hapa kesho nitasema sawa labda tumekuwa wapenzi tumekuja tumejibu ni wapenzi, utakosa swali la kutuuliza, unaweza ukatuuliza mtoto lini.Sisi tumeona tuwekeze kwenye kazi kwanza. Inawezekana tu kuwa na mshkaji kama huyu,” amesisitiza rapper huyo.

“Sababu wabongo unajua ukiwa na mtoto mkali tu inabidi mtu akae.”

The Amazing sasa wanafanya vizuri na wimbo wa ‘Umeniweza.’

Black Rhino awachana wasanii wanaotegemea kiki kwenye muziki


Rapper Black Rhino amewachana wasanii wanaotegemea kiki kwenye muziki wa Bongo Fleva ili wafanye vizuri.
Black amedai kuwa wasanii wengi wa kipindi hiki wamekuwa wakitegemea sana kiki ili ziwabebe kwenye muziki wa tofauti na ilivyokuwa kwa wasanii wa zamani.

“Wasanii wengi wa kuimba sasa wamekuwa wakitumia kiki wasanii wengi wamekuwa wakiwaiga wasanii wa Ulaya kutengeneza kiki kama hizo tofauti na wasanii wa zamani wengi walikuwa hawafanyi hivyo lakini muziki wao ulikuwa ukieleweka vizuri,” amekiambia kipindi cha Enews cha EATV.

Rapper huyo ameongeza kuwa kwa wale wasanii wanaotegemea kiki ipo siku watapotea vibaya na watabaki wasanii wanaofanya muziki mzuri.

Tunda Man: Cover la ‘Debe Tupu’ si dongo kwa Diamond

Tunda Man amefunguka kuwa cover la wimbo wake mpya ‘Debe Tupu’ halijamlenga mtu yeyote.
Kumekuwepo na maneno mengi yaliyozuka mitaani kuwa muimbaji huyo amemdiss hitmaker wa Salome kupitia cover ya wimbo wake huo inayomuonyesha paka akijitazama kwenye kioo na kujiona kama Simba.

Tunda amekiambia kipindi cha Dj Show cha Radio one, “Kitu kikubwa watu wanaangalia ile cover kwa jicho la tatu, waangalie kwa jicho la kawaida tu. Mimi paka niliyemzungumzia ni yule yule paka wa nyumbani na samba niliyemzungumzia ni yule yule wa Mikumi. Mtu anatoa zile tafsida nionekane nimemsema vibaya, kwahiyo wachukulie kawaida Tunda amemweka yule paka wa jikoni na Simba yule wa Mikumi wala sijamzungumzia mtu na debe tupu ni mwanamke au anaweza akawa ni mwanaume.”

Tunda ameongeza kuwa aliamua kutoachia wimbo wake wa ‘Mwanaume Suruali’ baada ya Mwana FA kumpigia simu na kumtaka asiachie kwa sasa wimbo huo kwa kuwa na yeye alikuwa anataka kuachia wimbo wake ‘Dume Suruali’ ili wasiwachanganye mashabiki.

Wanaomshauri Darassa akatae show zile wanazoziita za ‘vichororoni’ wanataka kumwigiza choo cha kike?


Darassa ni hadithi ya mafanikio ambayo kila mdau wa muziki ataikumbuka kwa mwaka 2016. Na hadithi yake ina funzo kubwa katika namna ambayo hit song hupatikana. Pengine nilichojifunza zaidi ni kuwa hakuna formula ya jinsi ya kupata hit.

Kwamba ‘don’t bother, just hit the studio do what you love’ mengine yatajulikana mbele ya safari, right? Kwasababu wakati mwingine ule wimbo ambao msanii aliurekodi kwa kujiachia tu studio kuwapa mashabiki wake zawadi, hugeuka kuwa mkubwa hadi humshangaza yeye mwenyewe. Na wakati mwingine, wimbo ambao msanii huuwekea mikakati mikubwa, kufanya uwezekaji wa kufa mtu na promo nzito, hugeuka kuwa ‘flop’ na ‘disappointment’ kubwa.

Kilichotokea mwaka huu kwa Darassa ni mawimbi ambayo kila kona imeyahisi. Muziki umegeuka kuwa wimbo wa hadhi ya ‘national anthem’ kwa muda mfupi. Ndio wimbo wenye rotation kubwa zaidi nchini kwa sasa. Huwezi kuukwepa. Usipousikiliza kwenye redio, utaona video yake kwenye TV. Usipousikia kwenye baa ya jirani, utausikia kwenye bajaj au bodaboda inayokatiza wakati ukitembea barabarani. Kwa ufupi katika mzunguko wako saa 12 za siku, uhakika wa sikio lako kuguswa na mawimbi ya mdundo wake ni mkubwa, utake ustake au labda uweke pamba sikioni.

Na kwa muda mfupi, Darassa amegeuka kuwa msanii wa rap mwenye show nyingi. Darassa amegeuka ‘hot cake.’ Hivyo inamlazimu kusafiri muda mwingi kwaajili ya kutumbuiza. Mfano siku kadhaa zilizopita alikuwa na show tatu katika mikoa miwili tofauti, Iringa na Shinyanga. Ni katika safari yake ya kutoka Kahama kwenda Kakola mkoani Shinyanga ndipo yeye na timu yake walipopata ajali ambayo kama si rehema za Mungu, angegeuka kuwa #hashtag.

Katika wakati huu ambao Darassa anafanya vizuri, amekuwa akipata ushauri mwingi kutoka kwa watu wanaotaka afike mbalimbali zaidi na kwamba asije siku moja akapotea tena baada ya kufika kwenye kilele cha mafanikio kimuziki. Hofu hiyo haikwepeki sababu kuna mifano mingi ya watu waliowahi kutoa nyimbo za ukubwa huo lakini leo hii wanapumulia mashine.

Miongoni mwa ushauri anaoupata ni kuwa apunguze show anazofanya kwa kuweka dau kubwa zaidi ili kuzichuja. Moja ya waliompa ushauri wa aina hiyo ni Sebastian Ndege, ambaye katika sehemu ya alichomshauri anasema, “Usichukue show za mapromoter uchwara waka dissapoint mashabiki wako kuwatia hasira na kukushusha hadhi. Bora ufanye shows chache lakini za ukweli, with detailed showcase.”

Mwingine ni Le Mutuz ambaye anamshauri kuwa ni muda wa yeye kuanza kuchukua malipo ya shilingi milioni 15 hadi 20. Na pia kuwapa masharti mapromota wa maeneo ya mbali kumtafutia usafiri wa ndege. Kwa upendo, wote, wametoa ushauri unaoweza kumjenga japo mwingine unakuwa ni nje ya uhalisia.

Nakubali kuwa kutokana na alipofika, Darassa hapaswi kulipwa kiasi kile kile kama ambacho alikuwa anatoza miaka miwili iliyopita, lakini hilo linapaswa kwenda kwa process. Ni haraka mno kutoka kulipwa mfano milioni 4 kwa show hadi kuwa milioni 20. Inahitaji justification zaidi ya kuwa na hits mbili kuweza kulipwa kwa ukubwa huo.

Watu wasimjaze maneno Darassa na kuanza ajisikie kuwa anapaswa kuanza kuchukua kiasi kile kile ambacho wasanii kama Diamond au Alikiba wanachukua – kumbuka safari ya wawili hawa na nguvu waliyojikusanyia hadi sasa. Hapo alipofika Darassa, kuna rappers kibao nyuma waliwahi kufika, lakini hawakulazimisha kupaa juu ghafla na kutaka walipwe mamilioni ya shilingi ambayo hayaendani na uhalisia.

Huu ndio muda ambao Darassa anaendelea kujijenga kujitengenezea ukubwa huo wa kutoza fedha nyingi au kuzikataa zile zinazoitwa ‘show za vichochoroni.’ Kumbuka kabla ya kuachia Muziki, hakuwa na ‘demand’ hiyo ya hata kuitwa kwenye utitiri wa show hizo. Show za milioni 3, 4 ndizo zinaweza kumjengea na kumtengenezea mazingira ya kudai shilingi milioni 15 au 20 kwa show moja baadaye. Hizi ni show zinazompa mtaji wa kujitengenezea himaya yenye nguvu itakayompa kiburi ya kukataa milioni 5 ili alipwe milioni 15.

Kuna wasanii wanaofanya vizuri ambao kupata show ya milioni 2 au 3 ni ngekewa, haiwezakani Darassa kuzikataa kisa ametoa hit ndani ya mwezi mmoja. Isitoshe, show za vichochoroni ndizo zinaonesha ukubwa wa msanii na dalili kuwa muziki wake umefika mbali. Ehh, ndiyo, haiwezekani kujiita msanii mkubwa wakati unajulikana mjini tu.

Ushauri wangu kwa Darassa ni kwamba aendelee kuwa mnyenyekevu hivyo hivyo kama alivyo sasa bila kuanza kuweka attitude kuwa hataki kwenda baadhi ya sehemu ambazo hazifikiki kwa ndege. Wanasema Roma haikujengwa kwa siku moja, ama hata mbuyu ulianza kama mchicha.. Ni process, inahitaji muda kutengeneza ukubwa, hauji ndani ya siku moja.

New Audio I Poison Feat. Mr T-Touchez - Kazi na Bata I DOWNLOAD


Official VIDEO | Mario Classic - Swagg | Watch


Official VIDEO | Wizkid - Daddy Yo (featuring Efya) | Watch


Official VIDEO | Zimwi Dzee Ft. Mr Blue, Billnass & Country boy - KIDON | Watch


Official VIDEO | Saxena Ft. Rich Mavoko - True Love | Watch


Official VIDEO | Viva Brain Ft. Juma Nature - Nakuhitaji | Watch


22 Des 2016

Madaktari wamshauri Darassa kupumzika baada ya kupata maumivu ya kichwa yaliyotokana na ajali

Rapa Darassa baada ya kunusurika kifo katika ajali mbaya ya gari akiwa na muongozaji wa video nchini Hanscana huko Kahama, Jamatano hii alienda katika hospitali ya Muhimbili jijini Dar es salaam kwaajili ya kucheki afya yake.
Akiongea na kipindi cha XXL cha Clouds FM Jumatano hii akiwa hospitalini hapo, Darassa alisema aliamua kwenda kucheki afya yake baada ya kuwa na maumivu ya kichwa yaliyotokana na ajali hiyo.

“Nipo hospitalini Muhimbili sasa hivi nawashukuru sana madaktari wa hapa wamenipokea vizuri wamenipa huduma nzuri sana,” alisema Darassa.

“Wamenicheki kwa sababu nilikuwa najisikia vibaya sana sehemu za kichwani nashukuru Mungu majibu yanaonyesha kila kitu kipo poa kabisa kuna damage ndogo wanaifanyia kazi naendelea na matibabu ila nimeshauriwa kupunguza mizunguko kwa wiki moja ili niweze kupumzika na kutibu hayo maumivu ya kichwa,”
Darassa na Hanscana pamoja na wenzao wawili alipata ajali hiyo wakati wakiwa njiani wakitokea Kahama mkoani Shinyanga kwenda Kakola mkoani humo kwaajili ya show.

Tangu nimefunga ndoa, sioni tabu naona raha tu – Mwana FA



Msanii wa muziki wa hip hop, Mwana FA amesema anayafurahia sana maisha ya ndoa tofauti na inavyodhaniwa na vijana wengi wenye uoga wa kuingia katika maisha hayo.

Rapa huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo Dume Suruali, amedai toka aingia kwenye maisha ya ndoa amekuwa ni mtu mwenye furaha zaidi.
“Ndoa siyo ngumu kama inavyofikiriwa na wengi, cha msingi muelewane, kila mtu ajue unachofanya, na kuheshimu nafasi yake ndani ya ndoa, maisha ya ndoa ni mzuri sana, tangu nimefunga ndoa, sioni tabu naona raha tu,” Mwana FA alikiambia kipindi cha FNL cha EATV wiki hii.
Mkali huyo wa wimbo ‘Bado Nipo Nipo’ aliyoitoa takriban miaka 7 iliyopita iliyokuwa ikitisha vijana kuoa, amedai aliyoyaimba katika ngoma ile ni ya kweli, na yalimsaidia kufanya utafiti wa kutosha kabla ya kuingia kwenye ndoa na ndiyo maana ndoa yake haina mambo kama yale aliyoyaimba katika ngoma ile.



Man Water atoa sababu zilizowafanya washindwe kumrudisha 20%


Mtayarishaji wa muziki nchini Man Water amefunguka sababu iliyowafanya washindwe kukamilisha mipango yao ya kumrudisha msanii wao 20% kwa mwaka huu.
Water amekiambia kipindi cha E-News cha EATV kuwa matatizo ya kufiwa ndio yalisababisha washindwe kukamilisha mipango yao kwenye muziki.

“Kwanza kabisa mipango ambayo tulikuwa tumepanga ilishindwa kutimia. Tulikuwa na mipango ya kufanya video na tunaangalia video ingekuaje, bajeti ipoje yaani kulikuwa na mambo mengi sana wakati huo huo 20% alifiwa na dada yake, mimi mwenyewe nikafiwa, yaani kulikuwa na mambo mengi sana hivyo kuahirisha kukawa kwingi sana. Unakuta upande mmoja kukiwa sawa kwingine kuna kuwa siyo, hivyo muda huu tunaomba Mungu mengine yasitokee yale ya dharura ili katika hii new page tujue tunafanya nini,” amesema Water.

Mtayarishaji huyo ameongeza kuwa mpaka sasa 20% ana nyimbo tano ambazo zipo tayari kwenye store yake. Mpaka sasa msanii huyo ameachia wimbo mmoja pekee tangu aliposaini mkataba na lebo yake hiyo ya zamani ‘Combination Sound’ mwezi Julai mwaka huu

Sallam aelezea zilipofikia collabo za Diamond na Rick Ross na Rihanna


Hivi karibuni wakati anahojiwa kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM, Diamond alitease ujio wa ngoma ambazo amewashikirisha wanamuziki heavyweight wa Marekani, Rick Ross na Rihanna.

Jumatano hii kupitia kipindi cha Campus Vibes cha Times FM, meneja wake, Sallam alifafanua zaidi kuhusu hatua iliyofikiwa ya collabo hizo. Sallam alidai kuwa collabo na Rick Ross imeshakalimika, huku ile ya Rihanna ikiwa kwenye hatua za mwisho kwakuwa tayari CV na historia ya Diamond imeshatumwa kwa uongozi wake kuweza kufikiwa maamuzi ya mwisho.
Kuhusu nyimbo alizoshirikishwa Diamond, Sallam alisema mwakwani itatoka ngoma aliyoshirikishwa na Burna Boy na Cassper Nyovest huku pia Dj Van wa Morocco akimshirikisha pamoja na msanii mkubwa wa Dubai.
Alidai kuwa kutokana na ubusy alionao hitmaker huyo wa Salome, imekuwa ngumu kupata muda wa kushoot video ya wimbo alioshirikishwa na msanii wa Jamaica, Alaine, wimbo alioshirikishwa na msanii wa Ivory Coast Serge Beynaud pamoja na kukamilisha wimbo anaoshirikishwa na rapper namba moja wa Cameroon, Stanley Enow.
Pia alidai kuwa Diamond atatumbuiza kwenye tuzo CAF 2016, Alhamis ya January 5, 2017 mjini Abuja, Nigeria na pia kwenye ufunguzi wa kombe la mataifa ya Africa (Total Africa Cup of Nations),itakayofanyika nchini Gabon kuanzia January 14.



New Audio I MIKE TEE Ft. CHEGE - UMENIKUTAGA I DOWNLOAD