burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

30 Nov 2016

Bifu ya Clouds Media Group na Lady Jaydee yamalizika

Baada ya takriban miaka minne ya uadui mkubwa, Lady Jaydee ametangaza kuwa hana tatizo tena na Clouds Media Group. Uamuzi huo umekuja baada ya Mkurugenzi wa Vipindi wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba kudai kuwa wapo tayari kuanza kucheza nyimbo za muimbaji huyo mkongwe iwapo atawapa ruhusa.
jide-na-ruge
Kujibu ofa hiyo, Jaydee alisema kauli ya Ruge ni ni sahihi na ya kiutuzima.
Muimbaji huyo mkongwe alitoa kauli hiyo kwenye mahojiano na mtangazaji wa Nyemo FM, ya Dodoma, Winston Makangale. “Nimeisikia kauli ya Ruge, kwa namna aliyoiongea na nafasi aliyokuwa nayo, sioni kama kuna kitu kibaya chochote alichokifanya kwa jinsi ambavyo amezungumza, naona amezungumza sahihi tu,” alisema.
“Hajanipigia simu na wala sijampigia simu, kwahiyo sio kwamba tumeongea kitu chochote lakini nayaona tu ni maamuzi ya kikubwa ambayo yamefanyika hapo. Hatujaongea kwasababu tulikuwa na mgogoro,” ameongeza.
Jaydee alisema uongozi wake ndio utakaokuja na maamuzi kufuatia ofa ya Ruge. “Kama kuna kauli yoyote ambayo itatakiwa kutoka, management itatoa kauli hiyo ya nini kitafuata.”
Na Jumatano hii kupitia kipindi cha Amplifaya cha Clouds FM, uongozi wa Lady Jaydee ulitoa taarifa yake rasmi kuhusiana na kuwa tayari kufanya kazi tena na kituo hicho.
“Hatuna tatizo na Clouds Media Group kuanza kupiga nyimbo za Lady Jaydee. Wanaweza kuanza kupiga wakati wowote watakapokuwa tayari kwakuwa chochote kilichotokea hapo nyuma kimefikia tamati, la msingi sasa ni amani na upendo vitawale,” yalisema maelezo yake.
“Kuanzia leo wana uhuru wa kupiga na kutaja jina la Lady Jaydee kadri wawezavyo.”
Wiki iliyopita kwenye mahojiano na kipindi cha XXL, Ruge alisema: Tatizo ni kwamba hakuna ambacho hatujamaliza, tulimaliza, tunasubiri order. Unajua kimsingi ulipopewa order ya kwamba ‘nyimbo zangu usipige, jina langu usiseme kwenye chombo chako, vyovyote itakavyokuwa mimi sitaki kusikia hiyo kitu’ hiyo ndio order. Kwahiyo labda tukikutana, nimuombe tena [Lady Jaydee] kama tutaruhusiwa kufanya hiyo kitu.”
Wiki kadhaa zilizopita Ruge na Joseph Kusaga walishinda kesi ya kuchafuliwa (defamation) iliyokuwa imefunguliwa dhidi ya Lady Jaydee na muimbaji huyo kuamriwa kuwaomba radhi.
“Tunashukuru walau tulishinda ile kesi lakini at least ilitengeneza mfano wa watu kuelewa kwamba tusipende kutuhumu vitu kama watu huna uhakika. Bahati nzuri pia hata katika hiyo kesi alisema mwenyewe hajawahi kusikia tunasema, aliambiwa na watu. Lakini ni mambo yashapita hayo.”

Joh Makini, Shettah, Ycee waipa nguvu remix ya Wabe ya P-Unit

Kundi la P-Unit la nchini Kenya linatarajia kuachia remix ya wimbo wake Wabe.
15306081_167776937022625_6669723429140168704_n
Kwenye remix hiyo wamewashirikisha Joh Makini, Shettah, rapper wa Nigeria Ycee na Kristoff.
Hata hivyo P-Unit hawasema remix hiyo itaachiwa lini.

Video: Nasry – Nimpende

Msanii Nasry baada ya kuwa kimya huu ndo ujuio wake tena amechia video mpya ya wimbo “Nimpende”, video imeongozwa na Lucca Swahili.


Nisha akanusha kupewa mimba na Nay wa Mitego

Baada ya msanii wa filamu Salma Jabu, Nisha kulalamika kubakwa na kupewa mimba na msanii wa muziki na baadaye kudai msanii huyo ameikataa mimba hiyo. Mashabiki katika mitandao ya kijamii walidhani mimba hiyo ni ya Nay wa Mitego hali ambayo ilimfanya rapa huyo kukanusha uvumi huo.
aaa
Nisha akionesha mimba yake
Rapa huyo kupitia kipindi cha U head cha Clouds FM amekanusha kumpachika mimba mrembo huyo huku akidai hajaonana naye kwa kipindi cha miaka 3.
“Mimi sielemi nimeshirikishwaje kwenye suala la mimba, tena naambiwa nimembaka, hivi mimi ninavyogombaniwa na wanawake naanzaje kumbaka?,” alisema Nay wa Mitego.
Baada ya kauli hiyo, muigizaji huyo wa filamu za vichekesho ameweka mambo sawa kupitia Instagram yake kwa kusema kuwa hakuwai kusema kuwa ana mimba ya mpenzi wake huyo wa zamani, Nay wa Mitego.
“Naywamitego iko hivi kabla hujaandika kitu chunguza sio unakurupuka tu na kuandika ujinga. Ulinisikia na kuniona wapi nimekutaja kwamba wewe ndo baby dady wangu???? hivi naanzaje kuzaa na wewe Nay?? kifupi pamoja na mapungufu na makosa yaliyojitokeza kwa baba k wangu humfikii hata kwa kucha labda umemshinda hizo tatoo zako kama bibi harusi. Nikuombe msamaha kwa kipi acha kudandia treni kwa mbele.??? tena watishe hao hao WANAUME SURUALI mimi simuogopi yeyote anayekojoa akiwa amesimama wala amechutama,” aliandika Nisha
sss


Hawa ni wasanii wa kuangaliwa kwa jicho la ziada

Ni miaka mingi tulikuwa tukilalamika kuhusu muziki wa Bongo Fleva lini utaweza kutambulika kwenye mataifa mengine huku nikikumbuka Salama Jabir alitumia nguvu kubwa kuponda video za wasanii ambazo zilionekana haziko poa.
c-d
Kiukweli ni ujasiri mkubwa aliufanya japo wapo baadhi ya wasanii wakubwa walimchukia kwa kitendo hicho lakini kwa asilimia kubwa amesaidia mpaka wasanii kuanza kutengeneza video nzuri na mpaka sasa tatizo hilo halipo tena.
Huo ulikuwa ni mwanzo nikikukumbusha kuhusu tulipotoka na muziki wetu japo kwa kidogo mpaka sasa tumefanikiwa kulifikia tobo tulilokuwa tunalitaka na hatimaye muziki wetu umepenya na kuanza kufanya vizuri kwenye mataifa mengine huku tukizidi kubarikiwa wasanii wenye uwezo mkubwa vipaji vikubwa kama Chemical, Ray Vanny, Darassa, Bill Nas, Barakah The Prince na wengine.
Hapa sitaki kwenda mbali sana ila nataka kusema kuwa kuna baadhi ya wasanii wanachukuliwa poa kwa sasa lakini endapo wakiangaliwa kwa jicho la tatu na wakipata support ya kutosha watafika mbali zaidi japo kwa sasa wameendelea kuchukuliwa kama ni wasanii wa kawaida tu.
Kati ya wasanii hao ni Darassa na Chemical. Wasanii haa wamekuwa wakichukuliwa kikawaida sana kwenye muziki lakini ni kazi kubwa wanaifanya hata ukifanikiwa kuangalia CV zao kwenye muziki tangu walipoanza kuachia ngoma zao wakiwa hawana zaidi ya miaka miwili tangu wafahamike lakini wameweza kuachia hit kibao na kuwashinda hata baadhi ya hao wasanii wengine wakubwa.
Hata ukiangalia kwa upande wa flow na style wasanii hawa wanatofautiana sana na marapper wengine ambao siku zote wamekuwa wakitumia style moja. Ukisikiliza nyimbo za Chemical kama ‘Sielewi’, ‘Kama Ipo Ipo Tu’ na ‘Mary Mary’ utaona kuna utofauti mkubwa zaidi upo kwenye hizi nyimbo zote tatu.
Vile vile kwa upande wa Darassa ambaye ameanza kuwanyima usingizi wasanii wengine wakubwa ukisikiliza ‘Sikati Tamaa’, ‘Tunaishi’ na ‘Muziki’ kuna utofauti mkubwa zaidi uliopo kwenye nyimbo zote.
Lakini pia ni ngumu kwa wasanii wengi kuachia hit tatu au zaidi mfululizo huku zote zikifanya vizuri kwa wati mmoja lakini kwa Darassa na Chemical imekuwa rahisi zaidi ndio maana wanatakiwa kuangaliwa kwa jicho la ziada kupitia hilo.
‘Kama Utanipenda’, ‘Too Much’ na ‘Muziki’ hizi zote ni hit za Darassa ambazo bado zinafanya vizuri zote kwa pamoja huku Chemical akiwa na ‘Forever (remix)’, ‘Am Sorry Mama’, ‘Kama Ipo Ipo Tu’ na ‘Mary Mary’.

HIZI KIKI JAMAN ZITATUTOA MAPOVU Nimefanya video karibia 10 lakini ya Diamond mnaniuliza kila saa, who is Diamond motherf**** – Tunda

Tunda amechoka kuulizwa maswali kuhusiana na kuonekana kwenye video ya Diamond ya wimbo Salome aliomshirikisha Ray Vanny.
14592013_1800456033544742_1978174817420967936_n
Ni kwasababu anajiuliza, iweje ameshaonekana kwenye video takriban 10, lakini tangu aonekane kwenye video ya Diamond, swali limekuwa lile lile na ni kama vile watu ndio wameanza kumuonea kupitia video hiyo.
14716636_1787141504900898_235544725296250880_n
Kutokana na kuchoshwa na swali hilo, Tunda anayedaiwa kurudiana na mpenzi wake Young Dee, amempa jibu kavu mtangazaji wa Jembe FM, Natty E aliyemrushia swali lile lile limkeralo.
“Nimefanya video ngapi? Nimefanya video karibia 10 lakini hii ya Diamond mnanifanyia interview kila saa,” Tunda alimjibu Natty.
“Diamond, Diamond, who is Diamond motherf*cker. Weka hiyo kwenye gazeti lako,” aliongeza.
15258734_1627592057542024_4426690412505202688_n
Natty alijikaza na kumjibu ‘Anyway, Unaweza acha hilo swali la kuhusu Diamond, it’s not a big deal.’
Tunda alijibu kikauzu zaidi, “Maswali yote jibu lake ndio hilo.”
Anachoshindwa kukielewa Tunda ni kuwa kushiriki kwenye Salome ya Diamond ni hatua kubwa zaidi katika career yake so far hivyo swali hilo hawezi kulikwepa! Hadi sasa video hiyo ina views milioni 9.2 na ni video ya Diamond inayopata views nyingi kwa kasi kuliko zote alizowahi kutoa.

Nick wa Pili akerwa na mashabiki kwenye muziki

Rapper Nick wa Pili amedai kuwa anachukia kuona mashabiki wakibishana kuhusiana na mambo yasiyo na faida kwenye muziki.
15056643_240347599718846_3937226945791524864_n
Akiongea na kipindi cha Ladha 3600 cha EFM Jumanne hii, hitmaker huyo wa Sweet Mangi amesema kuwa anafurahi akiona mashabiki wakibishana kuhusu muziki na ubunifu wa wasanii kwenye muziki wao.
“Mimi sikatai mashabiki kubishana ila wabishane kuhusu muziki sio nani kakaa wapi anafanya nini. Ningefurahi kama wangebishana kuhusu show, ubunifu,” amesema.
“Unapoona mtu amesema fulani namba moja huna haja ya ‘Kudebate’ hii inatokana na maoni vile ambavyo mtu anaona na anapima kwa vigezo vyake. Msanii wa Hip Hop anapokuwa na top track sote tunapaswa kufurahia,” ameongeza.

Jokate athibitisha rasmi uhusiano na Alikiba kwa salamu hizi za Birthday

Uhusiano wa Jokate na Alikiba una takriban miaka miwili sasa lakini hakuna hata mmoja aliyewahi kukiri hadharani.
15057329_103326730157312_6452928082926895104_n
Waswahili husema penzi ni kikohozi, kulificha huwezi. Ndio maana pamoja na kujitahidi sana kuuficha, uzito wa penzi lao umekuwa ukiacha mianya mingi inayodhihirisha uwepo wake mbele ya hadhira.
Na sasa huenda Jokate akawa ameuweka wazi zaidi kwa salamu za birthday alizomtumia mpenzi wake huyo aliyesherehekea siku yake ya kuzaliwa, November 29.
Akijaribu kutomwaga mchele kwenye kuku wengi, Jojo ametumia lugha ya Kifaransa kuwasilisha ujumbe wake.
jokate
Shabiki mmoja anayeielewa lugha hiyo ametafsiri post yake kwa Kiingereza inayosema:
Baby happy birthday I love you so much,it is paining,I hope that the French has sang you prepare for that, but I want nothing,but the best for you from the bottom of my heart the rest I leave to God for what happens to know that Jojo doesn’t disturb and that am happy to have you as my friend,rest blessed

Alikiba adaiwa kumtupia dongo Diamond baada ya kuandika amewaona ‘Simba Original’

Jumanne hii ilikuwa ni birthday ya mkali wa wimbo Aje, Alikiba ambapo aliungana na uongozi wake kwenda mbuga ya wanyama ya Serengeti National Park kwa ajili ya kusherekea siku hiyo muhimu katika maisha yake.
rayx
Alikiba akiserebuka na mrembo mmoja wa kizungu
Hata hivyo mkali huyo amechafua hali ya hewa mitandaoni baada ya kuposti picha yake wakati akisherehekea siku yake ya kuzaliwa na kuandika maneno kuwa anawaangalia Simba Original ambapo ujumbe huo umetafsiriwa kama kijembe kwa staa mwenzake Diamond Platnumz ambaye naye ujiita Simba.
zzzzaa
Haya ni baadhi ya maoni ya mashabiki hao katika mitandao ya kijamii.
pius_____himself
Kumbe we @officialalikiba ni pimbi tu, achana na hizo mambo za kiki braza piga kazi.. Unataka tu watu waseme
ts_zizahTeam
kitunguu buana ss mtu kaona simba original hamtaki aseme mnataka aandike tumbili au nungunungu huku hatutafutagi kiki bwana kik tunayo toka 2010 tulivyoimba na R kelly so kajambeni mbele huko #simbaoriginal
h_wa_wcb
Mbona unapiga vijembe baada ya kupiga kazi au kwakua umekaribishwa kwenye busta na wewe upate kiki jenga nyumba usijenge majungu@officialalikiba

ms_ticky

Hahahahha @officialalikiba watu wanatokwa mapovu hatari… Mie namuona simba OG sasa Povu la nn… Wamepanick balaaa
tony_k_tz
@mcute_mcute njoo umuone cmba original simba anaish polin cio mjin😂😂😂😂
jennifernatubhai
@zero2hero3 ahahaaaa yaan mtaishia kuongea tu lkn maisha ya kiba hamtayajua ng’ooo kwasbb sio mpenda sifa mbona siku iliyoonyeshwa nyumba yake povu liliwatoka? Eti anawatt wengi wengine alizaa na ww? Naisitoshe kwani alishakuomba kibaba ili watt wake wale? Kajiandaee

Mrembo huyu ndiye anayeutuliza moyo wa Rayvanny wa WCB?

Ule usemi wa Kiswahili unaosema ‘penzi ni kikohozi kulificha hauwezi’ unazidi kujidhihirisha kwa muimbaji wa WCB, Rayvanny baada ya anayedaiwa kuwa mpenzi wake kuonyesha ni jinsi gani anavyomzimia mkali huyo wa wimbo, Sugu.
rayx
Fahyma 
Mwaka huu mwanzoni Rayvanny alipost picha mtandaoni akiongelea na mrembo huyo hali ambayo iliibua maswali mengi kutokana na picha hiyo kutoonyesha sura ya mrembo huyo.
yrat
Muimbaji huyo hakuwahi kuzungumza chochote kuhusu mrembo huyo, lakini binti huyo anayedaiwa kuwa ni mpenzi wake ameamua kufunguka kupitia mtandao wa instagram kuonyesha jinsi gani anampenda mkali huyo wa wimbo, ‘Natafuta kiki’.
“Nakupenda sana mumewangu hakuna wakufanana na wewe mm bado sijaona 💑,” aliandika instagram mrembo huyo huku akiwa amepost picha hapo chini.
ray-vanny
rayvanny


LITUNZE JICHO LAKO LILINDE LIKULINDI NA KITU HII APA.............!!!

Jicho ni kiungo muhimu kukulinda kwa ajili ya maisha bora FOREVE VISION ina bilberry,luteina,zeaxanthin na anti-oxidants

BILBERRY inasaidia kulifanya jicho lione vizuri na kusaidia mzunguko wa damu kwenye jicho 

LUTEIN NI CAROTENEID inayotokana na mboga mboga na matunda kazi yake kulinda retina ya jicho ZEAXANTHIN NA ASTAXANTIN ni Carotenoids zinasaidia ufanyaji kazi ya misuli ya jicho 

FAIDA za hii BIDHAA ni nyingi mno 
Husaidia macho kuona vizuri 
huboresha mzunguko wa damu kwenye macho 

WASALIANA NAMI KUPITA HII NAMBA
0684016994
&
0767616698
&
0718223749
KWA USHAULI ZAIDI

Msanii Jobfire wa Melody Aachia Ngoma ya Funga mwaka



Msanii anekuja kwa spidi kama moto wa kifuu hivi siku chache zilizopita aliachia ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la NI SAWA  imeonekena kuwabamba wengi na kusikika kwenye vituo mbala mbali vya redio
kama hukuisikia hii ngoma ni wakati wako sasa gusa kwa HAPA kuipata

29 Nov 2016

Headlines mpya za Young Dee kurudiana na Tunda


U Heard ya Soudy Brown ndani ya XXL ya Clouds FM iko na story kuhusu uhusiano wa kimapenzi uliokuwepo kati ya rapa Young Dee ambaye aliwahi kuwa na uhusiano na Video Queen Tunda waliyeacha baada ya kutoelewana kupelekana polisi.
Baada ya kuwepo taarifa kwamba Tunda ameachwa na mwanaume anayetajwa kuwa alikuwa akimgharamia kwa kila kitu ikiwemo kulipia nyumba, kununua magari na starehe zote alizokuwa akizifanya kila siku, ikaja kuonekana ameanza kuwa karibu tena na Young Dee.
Leo Soudy Brown amepiga stroy na Young Dee ambaye ameeleza kuwa yeye na Tunda wako vilevile kama mwanzo hawakuwahi kugombana na ameamua kumsamehe Tunda kwasababu itakuwa kosa kubwa endapo hatamsaheme wakati yeye pia ana makosa makubwa zaidi ya hayo ya Tunda.
“Mimi nilikuwa na matatizo yangu mengi sana hata kufika hapa tu nimesamehewa sana vitu vingi katika watu ambao hawakutakiwa kusamehewa ni mimi ndio mana nimeamua kumsamehe, kwa yote ambayo Mungu amenisamehe nisiposamehe nitakua nakosea sana” – Young Dee

Kidogo ya Diamond na P-Square yashinda tuzo Nigeria, AELA

Diamond Platnumz ameshinda tuzo ya African Entertainment Legend Awards (AELA), za nchini Nigeria kwenye kipengele cha Best Collaboration (Africa) kutokana na wimbo wake Kidogo aliowashirikisha, P-Square.
14561853_125294524622138_3682255086983053312_n
Tuzo hizo zimetolewa Jumapili hii jijini Lagos, Nigeria.
Kuhusu AELA
African Entertainment Legend Awards (AELA) is designed to recognize and celebrate personalities and entertainers who standout distinctively and remained consistent overtime in their various fields of entertainment. AELA is also geared towards giving support to young emerging and creative talents in Africa and Diaspora.
African Entertainment Legend Awards (AELA) is produced and packaged by Flexy Entertainment with the support and collaboration of Africa’s finest brands and entertainment lovers. It is an annual celebration of the most distinguished African Acts, in Music, Film production, Movies, Comedy , On Air personalities ,Brands, Entertainment Personalities, Broadcasting, Comedy, Fashion, Media, Modeling and Magazines.
It is indeed about blitz, style, glitz, razzmatazz and celebrating legends and true excellence in creative arts across Africa and diaspora.
This is undoubtedly the first and the most prestigious legendary award bringing African Entertainers, Government personalities, Organisations and Brands under one roof to be celebrated for their enormous contributions to the development of entertainment in Africa.

Alikiba aicheka kauli ya Diamond kuhusu pete ya kijani!

Je unaikumbuka kauli ya Diamond aliyoitoa wiki iliyopita kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM kuhusu pete ya kijani?
15056662_331170897262349_6840282975670632448_n
Ngoja nikukumbushe japo kidogo kile alichokisema, “Mimi sina matatizo na watu ndio maana wakijaribu kushindana na mimi huwa wanashindwa. Hata ukiniangalia sina hata pete ya kijani kwenye vidole vyangu.”
Kumbe alikuwa amerusha jiwe gizani kwa upande wa pili. Inawezekana Alikiba ameshtuka hilo kutokana na picha aliyoiweka kwenye mtandao wa Instagram na kuandika, “Pete Ya Kijani 😂😂#BirthdayLoading29thNoV #KingKiba.”
15101765_1872147946350780_2002734140499165184_n
Mwanzo ilionekana ilikuwa ni vita baridi ya maneno ya chini kwa chini kati ya mafahari hao lakini kwa sasa hakuna kilichojificha tena na kila kitu kipo wazi.
Wiki iliyopita hitmaker huyo wa Salome na Ommy Dimpoz walichafua hali ya hewa kwenye mtandao huo kwa kutupiana vita ya maneno ya kejeli na kukashifiana.

Kufungiwa kwa Chura kulinipa msukosuko lakini niligoma kukata tamaa – Snura

Snura anasema kipindi ambacho wimbo wake Chura unafungiwa kilikuwa cha misukosuko lakini aligoma kukata tamaa.
15034852_1198217740265763_8711447471730982912_n
Akizungumza na mtangazaji wa Kings FM, Prince Ramalove, Snura alisema neno kukataa tamaa halipo kwenye orodha ya msamiati wake.
“Kwenye suala la kukataa tamaa kwangu halipo,” alisema. “Na kama ningekuwa ni mtu wa kukataa tamaa ningekata tamaa kwenye Chura, lakini sikukataa tamaa hadi kuhakikisha nairudisha na masekeseke ya chura yale yaliyotokea yangenikatisha tamaa. Nimekutana na mambo mengi sana kuhusiana na chura,” alisema.
Snura anasema hasara iliyopatikana kutokana na kufungiwa kwa chura ilikuwa kubwa kwakuwa ilikuwa na dalili za kuwaingizia fedha nyingi kwenye Youtube ukiachilia deals zingine za show.

Jux afunguka kuhusu timu zilizopo kwenye muziki

Jux amefunguka kuhusu timu zilizopo kwenye muziki hapa nchini. Hivi karibuni timu hizo zimeonekana kuchafua hali ya hewa mitandaoni kwa kutukanana matusi mazito huku baadhi ya wasanii wakikumbana na mvua hizo za kashfa na matusi.
14624632_579954458855754_2472429113994903552_n
Hitmaker huyo wa Wivu, amemuambia mtangazaji wa Maisha FM ya Dodoma, Silver Touchez kuwa timu zinasaidia wasanii kufanya vizuri ila hazitakiwi kufika mbali zaidi hadi kutaka kushikana mashati.
“Muziki wetu sometimes unakuwa unalala sana, unatakiwa uchangamke. Unajua kunapokuwa na timu hata msanii unayekuwa unashindana naye kazi zinakuwa zinafanyika kwa ubora mtu anakuwa hakuchukulii poa. Lakini kitu ambacho sikipendi kwenye hizo timu zisifikie hatua zikaanza kushikana mashati, kuchomana mavisu sijui nini,” amesema.
“Mimi mwenyewe na Ben Pol ni wapinzani wakubwa tu, lakini tukitoka kwenye stage au studio ni washkaji lakini kikazi akitoa video ananiambia kaka nimeshakunyoosha na mimi namuambia utaona,” ameongeza.

Fid Q na Joh Makini waeleza kwanini hawajafanya collabo hadi sasa (Audio)

Kama wewe ni shabiki wa hip hop, bila shaka utakuwa na hamu ya siku moja kuwasikia Joh Makini na Fid Q kwenye ngoma moja. Kwanini hadi sasa hawajafanya wimbo pamoja?
fid-22
Mtangazaji wa Jembe FM, JJ alizungumza na rapper hao waliokuwa pamoja jijini Mwanza kuhusiana suala hilo.
“Collabo hiyo bado haijashindikana nadhani bado haijafikiriwa tu lakini muda wake ukifika itafanyika,” alisema Fid.
Kuhusu anavyowachukulia Weusi, Fid alisema, “Wanafanya kile kitu wanachokiamini na kinawalipa na hiyo ndio sanaa yenyewe, fanya kitu ambacho unaamini. Usifanye kwasababu mtu fulani anafanya au mtu fulani kakuambia fanya,” aliongeza Fareed.
Kwa upande wake Joh Makini alisema, “mimi nafikiri ni time tu, muda ndio unasema wakati mwingine. Sababu hatujawahi kuwa na tatizo naye, watu wengine wanachukulia hivyo. Mimi nafikiriaga ni kama ushindani tu wa kwenye muziki ambao lazima uwepo ili kuongeza utamu. Lakini no hard feeling, anytime pengine.”

Maua Sama afikiria kumleta muongozaji wa nje kwaajili ya video ya ‘Sisikii’

Maua Sama amekiri kuwa video ya wimbo wake Sisikii imechelewa kutoka lakini mpango wake ni kumleta muongozaji wa nje kwaajili ya kazi hiyo.
14730740_738420099643409_1139081384812347392_n
“Tunaifanyia hapa hapa Tanzania ila tulikuwa tunafikiria mimi na management yangu tulete director kutoka wapi,” Maua alimuambia mtangazaji wa ABM Radio ya Dodoma, DJ Rodger.
Kwa upande mwingine anasema sababu nyingine ya kuchelewa kwa video yake ni kutokana na kuwa ni wimbo uliovuja. Hata hivyo amesema mpango wa kuifanyia video upo pale pale.

Kauli ya Ruge ni sahihi na ya kikubwa, uongozi utaifanyia maamuzi – Lady Jaydee (Audio)

Laydee amesema kauli aliyoitoa Mkurugenzi wa Vipindi wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba kuhusu kuwa tayari kucheza nyimbo zake akiwaruhusu, ni sahihi na ya kiutuzima.
jide-na-ruge
Muimbaji huyo mkongwe ametoa kauli hiyo kwenye mahojiano na mtangazaji wa Nyemo FM, ya Dodoma, Winston Makangale.
“Nimeisikia kauli ya Ruge, kwa namna aliyoiongea na nafasi aliyokuwa nayo, sioni kama kuna kitu kibaya chochote alichokifanya kwa jinsi ambavyo amezungumza, naona amezungumza sahihi tu,” alisema.
Amesema yeye na Ruge hawajahi kuzungumza kwa miaka minne sasa.
“Hajanipigia simu na wala sijampigia simu, kwahiyo sio kwamba tumeongea kitu chochote lakini nayaona tu ni maamuzi ya kikubwa ambayo yamefanyika hapo. Hatujaongea kwasababu tulikuwa na mgogoro,” ameongeza.
Jaydee amesema uongozi wake ndio utakaokuja na maamuzi kufuatia ofa ya Ruge.
“Kama kuna kauli yoyote ambayo itatakiwa kutoka, management itatoa kauli hiyo ya nini kitafuata.”

Selfie ya Diamond akiwa na kiboxer yasababisha povu zito Instagram

Diamond Platnumz ni bingwa wa kusababisha povu kwenye mitandao ya kijamii. Jumanne hii alisababisha tafrani kwenye mtandao wa Instagram baada ya kupiga stunt kama ya The Game na Kevin Hart, kwa kupost selfie akiwa amevalia kiboxer cheusi.
14561815_1832954966923592_3538369615233024000_n
Kwenye picha hiyo, Diamond aliandika: Straight from the Changing room!…I think i need to go back to the gym so that i can be more flexible on m 24th Pre-XMass Parformance in Dar Es Salaam.
Licha ya kufunika kwa emoji kwenye eneo la sehemu zake za siri, selfie hiyo imesababisha hisia tofauti huku wengi wakimponda staa huyo kwa kukosa staha.
Hizi ni baadhi ya comments:
isaac_siame: @diamondplatnumz sitaki kuamini kama mawaziri kama nape au makamba watatamani kuja tena wcb kuonana namsanii wa namna hii, hii itakucost au imekucost tayari @babutale busara zako azijatumika kushauri hii naanza kuona misingi ya heshima ulioitunza kwa mda mrefu ikipotea
tausizehemasaleh: You ‘ve a beautiful soul but I think sometimes you go over board,remember to much is given .much is expected,I respect the path Mom Tee is taking,don’t neglect her advices,you may need them sometimes,Big love small bro
yahyakiwera8646: Nduguyangu nakuusia usidanganyike nahizi like nacomment kumbuka weweni muislamu nautazikwa kiislamu kuogope mungu kwanza niharamuvhizo tatoo ukiswali swalazako haziswihii ukiogajanaba halitoki nduguyangu unapotea HAWA wanao like wote kaburini hatakuwepo utakua pekeyako namatendoyako iwemazuri au mabaya je utaponaa? Ilahuu WANGU niukumbushotu kwako nikutakie mabadiliko usijekusema hukuambiwa buree miminisha kuambia
swaum1140: Mmmm jaman mm hapo hapan nasibu sio nzuri hyo pic kwa kweli kumbuka wew ni baba now sio pich nzur kumbuka IPO cku tifa ataiona alaf itakua aibu kubwa uxifany hvy bhana hapo mm sijapenda kabisaaa
ommie_latino26: Bro huo ni ujinga una familia sasa ina maana hapo tiffah aje aone dudu ya baba au
its_mancrowdtz: Endeleeni kukaa uchi kusuka kuchora tattoo na upuuzi mwngne..kibaya zaidi watu wanawafuata nyinyi km ma role model kwahy dhambi atakayofny kwa kuwaiga nyie mnaandikiwa na nyinyi…mtu anaefanya uovu hadharani ana hasara kubwa kuliko yule anaefny kwa kujificha@officialalikiba@diamondplatnumz😭😭Allah awaongoze kwakweli
nelyhassan: Huyu ni shetani hata muziki siku hizi hana pole kaka umebadilika sana sio diamond yule wa kitambo duh huruma jamani

New Audio I Navy Kenzo Ft. Wildad - Feel Good I DOWNLOAD

New Audio I Orbit Ft. Sumawani - TAKE ME HIGH I DOWNLOAD

Official VIDEO | Navy Kenzo Ft. Wildad - Feel Good | Watch



New Audio I Rocky ft Orbit -Crazy Foy You I DOWNLOAD

New Audio I Top B ft Jobfire wa melody-sijashikiwa I DOWNLOAD

Exclusive Interview Ndani ya KIBO FM na Jobfire wa Melody[SAUTI ZA MATUKIO]

Msanii machachali toka pande za kilimanjaro anaefanya vizuri ni kazi yake mpya inayotambulika kwa jina la NI SAWA  anaekwenda kwa jina la Jobfire wa melody au waweza mwita sauti za matukio 

Jobfire wa melody amesema kesho siku ya jumatano tarehe 30 atakuwepo ndani ya kibo fm kuitambuisha ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la ni sawa pia jobfire wa melody hato kuwa pekee ake atasindikizwa na wasaa wakali toka kilimanjaro akiwemo TOP B dhahabu ya kaskazini bila kumsahau JAY WA LEO PLUS na wengine wengi hii si ya kuikosa mtu wangu wa nguvu

Jobfire wa melody ameiambia g.lovetz kwamba kwa sasa anahakikisha usambazaji wa nyimbo wa nyimbo yake mpya unakwenda sawa 

26 Nov 2016

New Audio I Darassa Ft. Ben Pol - Muziki I DOWNLOAD

Official VIDEO | MwanaFA Ft. Vanessa Mdee – Dume Suruali


dume
djmwanga1bdownloadlogo

Ommy Dimpoz afunguka kisa cha kukosana na Diamond Platnumz

Katika interview ndefu aliyofanyiwa Alhamis hii kwenye kipindi cha XXL kupitia Clouds FM, Ommy Dimpoz amefunguka kwa kina visa na mkasa vilivyopelekea akosane na swahiba wake wa zamani, Diamond Platnumz.
Ommy amelazimika kusimulia hayo baada ya Jumatano kupitia kipindi hicho hicho, Diamond kuelezea uhusiano wao na jitihada ambazo Ommy amewahi kuzifanya ili kuomba wayamalize.
Hitmaker huyo wa Wanjera amesema katika urafiki wao wote na Diamond, ni yeye ndiye alikuwa mwaminifu (loyal) zaidi katika kuuenzi lakini kuna wakati mwenzake alianza kuonesha kumficha baadhi ya vitu hasa vinavyohusiana na kazi.
Amesema mara zote alikuwa akimshirikisha kwenye mipango yake ikiwa ni pamoja na kumsikilizisha nyimbo zake kabla ya kutoka ili kumuomba ushauri na kutolea mfano alivyomsikilizisha wimbo wake Tupogo na kumweleza kuwa amepanga kuongeza vionjo vya saxaphone kwa kumtumia King Malou. Hata hivyo anadai kuwa siku chache baadaye alishangaa kumkuta Diamond akiwa na mpiga saxaphone huyo akiingia kionjo kwenye wimbo wake ‘Number 1’ katika studio za MJ Records.
“Nikajiuliza kuwa pengine labda alikuwa na wazo kama hilo, sikutaka kujiuliza mengi, unajua sometimes ukijiuliza mengi utaenda far zaidi, nikauchuna tu,” alisema Ommy.
Anasema baadaye alisikia akimuambia Marco Chali kuwa amchomee CD kwakuwa anasafiri na walipomaliza Ommy alimuuliza kuhusu safari hiyo lakini Diamond alimuambia kuwa alikuwa akimdanganya tu producer huyo wa MJ Records na kwamba hakuna safari yoyote.
“Kesho yake naona anapost picha yupo kwenye ndege, nikajiuliza ‘huyu si nilimuuliza jana kama anasafiri, si ni mwanangu’, nikasema anyway labda ni safari imejitokeza ghafla you never know,” ameeleza Ommy.
Baadaye mshkaji wao Halima Kimwana alikuja kumwambia kuwa Diamond alienda Afrika Kusini kufanya video yake kitendo kilichomwacha na maswali mengi lakini anadai alipuuzia. Amesema baada ya muda ndipo Diamond alipofanya uzinduzi wa video ya Number 1 na yeye mwenyewe kualikwa.
Amesimulia tukio jingine ambalo lilimuumiza ni baada ya kumuomba Diamond waende pamoja Marekani kwenye tuzo za Afrimma kwa gharama zake mwenyewe ili amsaidie kumtafutia connection.
“Sasa kila siku nikiuliza safari lini naona mtu anaingilia huku anatokea huku.”
Anadai swahiba wake huyo aliendelea kumchenga hadi alipokuja kugundua amesafiri bila kumwambia na siku hiyo akawa hapokei simu zake. “Baada ya kupita masaa mengi, jioni anakuja kunicheck yuko transit South Africa ‘mwanangu ilitokea ghafla nikasafiri.’ Kwahiyo nikajiuliza nikasema hapa kuna style za kupunguzwa. Kibinadamu unajua lazima uchekeche.”
Ommy pia alielezea jinsi ambavyo alikuwa mtu wa kwanza afanye collabo na Davido na alikuwa tayari kutoa $3,000 lakini baadaye Sallam, meneja wa Diamond, alikuja kumweleza kuwa Dangote yupo tayari kutoa $5,000 ili wafanye naye. Anasema aliachana na collabo hiyo na kutafuta nyingine na Iyanya ambayo nayo pia alikuja kugundua baadaye rafiki yake huyo ameshaiwahi.
Hata hivyo Ommy amedai kuwa kitendo cha yeye kumtumia Wema Sepetu kwenye video ya Wanjera ilikuwa kama sababu tu ya Diamond kuvunja ushkaji wake. Amesema ni kwasababu amekuwa na urafiki na Wema hata kabla ya kukutana na Chibu na kwamba hadi ‘first kiss’ yao aliishuhudia kwa macho yake.
Ommy ambaye jina lake ni Omari Nyembo, amesema kukosana kwao hakukuwa sababu ya yeye kumchukia pia Wema kwakuwa urafiki wao haukusika na kwamba kipindi Ommy anaenda SA kufanya video hiyo, Wema alikuwa na uhusiano na mwanaume mwingine na kukanusha kuwahi kutoka naye kimapenzi.
“Kwahiyo nikaona kuna suala lilikuwa kwamba mtu ametafuta sababu. Hebu niambie Wema amekuwa na mahusiano na watu wangapi wengine ambao leo hii bado unaona D yuko nao close? Kwanini nilipokuwa naye mimi tu ndio imekuwa tatizo?” amehoji staa huyo.
Kuhusu tuhuma za kutaka ‘kupumuliwa’ zilizotolewa na Diamond kwenye post yake ya Instagram dhidi yake, Ommy amesema pale ‘mtu anapotaka kukutana hakuchagulii tusi.’
“Sometime unapoitoa kauli, huwezi kujua itamwathiri mtu kwa kiasi gani, pengine itamwathiri kwa kiasi kikubwa kwasababu kuna mtu ataichukua ile kauli kiushabiki. Hata kwenye comments, mimi ninaweza kuzima comments zangu kwenye Instagram lakini nimeziacha na ukisoma comments utaona kabisa mwingine anakutukana ‘we shoga.’ Lakini as long as mimi ninajua mzima hainiathiri, kwanza hakuna tusi jipya, imeanza kutukanwa mimba!”

Diamond atoa jibu la utata kufuatia interview ya Ommy Dimpoz

Inaitwa Tit for Tat! Baada ya Ommy Dimpoz kueleza kwa kina kuhusiana na sababu iliyopelekea wakakosana na Diamond, muimbaji huyo wa Salome, amejibu kupitia Instagram.
15056662_331170897262349_6840282975670632448_n
Majibu ya Diamond ni ya mafumbo kiasi na tayari yamepokelewa kwa hisia tofauti na mashabiki huku wengi wakichukizwa na kauli yake.
Ameandika:
Basi nlivyokuwa Mshamba Nikajua Mtu Mwenye Roho Mbaya na Mbinafsi Mungu ndio Humuadhibu na Kumfelisha kwa Roho Mbaya lake ili asifanikiwe… halaf Mwenye Roho nzuri Mungu Humlipa kwa Kumfanya afanikiwe zaidi na zaidi…. Asa nashangaa Mwenye Roho Mbaya eti Mungu ndio Kamfanikisha, halaf Maskini ya Mungu Mwenye roho nzuri eti Miguu juu…..au pengine labda Mwenyez Mungu kakosea kidogo kwenye Mahesabu yake..???😟 hii nayo ni #KOKORO ujue
Itazame hapo chini interview ya Ommy Dimpoz.


Ommy Dimpoz: Nilichangia kuandika Nasema Nawe ya Diamond

Ommy Dimpoz amesema alichangia kuandika hit single ya Diamond, Nasema Nawe – kipindi bado ni marafiki.
“Mimi nataka kusema kitu kimoja, sijawahi kusema sehemu yoyote hapa, mfano kwenye nyimbo ya mduara ya D Nasema Nawe, mimi nimechangia kwa asilimia kubwwa uandishi wa ile nyimbo. Sio kwamba D hajui kuandika, anaandika vizuri na nawaheshimu ni moja ya waandishi bora kabisa,” Ommy alikiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM, Alhamis hii.
Ametolea mfano mstari aliochangia ni wa verse ya pili usemao ‘zingifuli zingifuli usozinga mahala ukakaa.’ Muimbaji huyo amesema hata kwenye verse ya kwanza kuna maneno ameyaandika lakini hakuwahi kutaka apewe credit.
“Sikufanya vile kwasababu nilipwe au nipewe credit. Lakini nataka tu niseme kuwa mashabiki kuna vitu vingine vingi hawajui,” alisisitiza.

Wema Sepetu ampongeza Ommy Dimpoz

Baada ya hapo jana Ommy Dimpoz kufunguka kiundani kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM kwa kuelezea kilichopelekea akosane na rafiki yake wa zamani, Diamond Platnumz – Wema Sepetu amempongeza kwa kile alichokifanya.
dimpozzz-25f2a
Malkia huyo wa filamu nchini, amempongeza hitmaker huyo wa Kajiandae kwa kumsifia kuwa ni mpole na mwenye busara ila alipenda kile alichokifanya kwenye mahojiano yake hayo.
Kupitia mtandao wa Instagram, Wema ameandika.
Busara, Upole, Hekma… Thats wat u r made of… Im very very Proud and Impressed kwakweli… Mnyonge mnyongeni haki yaki mpeni… Sasa sio mje muanze kusema sijui napick sides… Nooooo…!!! Sina side maana na mimi pia ni outsider tu… But kwa leo nimependa ulichofanya Ommy…. Forever Bae… 👌🏽Sometimes being the bigger person doesnt hurt… @ommydimpoz