burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

21 Jan 2018

BARAKAH THE PRINCE AKERWA NA UDHALILISHAJI WA ANAYEJIITA NABII, AOMBA ADHABU YA KUNYONGWA


Msanii wa muziki kutoka Tanzania, Barakah Andrea ‘Barakah The Prince’ amekerwa na vitendo vya mtu aliyejitambulisha kwa jina la Nabii Tito anayesambaza ujumbe na kufanya ibada sambamba na ulevi kwa msisitizo wa matumizi ya pombe na kuoa wanawake zaidi ya mmoja kwa kivuli cha uamini wa Mungu.

Kupitia ukurasa wa Instagram Barakah ameweka kipande kifupi cha video ya Nabii huyo akiendesha ibada kwa mifano ya kuonesha kwa uhalisia matumizi ya pombe na mapenzi kwa mwanamke zaidi ya mmoja ambapo Barakah ameviomba vyombo husika kumchukulia hatua kali za kisheria ili kukomesha hali hiyo anayoendelea kushamiri kwani ila kila dalili za udhalilishaji, kinyume na tamaduni na Desturi za mtanzania.

“Kama ningekuwa na mamlaka katika Nchi hii basi uyu mtu ningeandaa sherehe ya kitaifa ya KUMNYONGA mbele ya mamilion ya watu..Tucheze na vyote na sio kucheza na imani ya watu,na kudhalilisha wanawake ambao ndio mama zetu..enyi vyombo husika hii ipo nje ya maadili ya taifa letu..ningependa uyu bwana apewe adhabu niliyoiomba hapo juu..na ifanyike sherehe kubwa ya kitaifa..” Aaliandika Barakah.

Miaka 14 jela sio mchezo, lazima tuwamiss mashabiki – Papii Kocha na Babu Seya


Muimbaji nguli wa muziki wa dance, Nguza Viking maarufu kama Babu Seya pamoja na mwanae, Papii Kocha wameanza maandalizi ya ujio wao mpya, ikiwa ni takribani miaka 14 tangu waachie kibao kipya.

Wawili hao walipewa msamaha na Rais Dkt John Magufuli kwenye maadhimisho ya miaka 56 ya Uhuru. Serikali imeonesha nia ya kuwasaidia waimbaji hao wanaopendwa sana kurejea tena kwenye muziki kwa kishindo.

Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Bi. Juliana Shonza aliwakutanisha na uongozi wa Wanene Studios waliokubali kuchukua jukumu la kuwarudisha tena kwenye muziki. Tayari wameanza kuingia studio kuandaa kazi mpya katika studio hizo kubwa na bora zaidi katika ukanda wa Afrika Mashariki na kati.

Wameanza kwa kufanya photoshoot, kitu ambacho wamekiri kuwa ni kigeni mno kwao kutokana na kuwa gerezani kwa miaka 14 na wametoka katika nyakati ambazo muziki wa Tanzania umepiga hatua kubwa ukilinganisha na zamani.

“Miaka 14 si mchezo, mambo kama haya si unayaona mwenyewe, niliyamiss, nimemiss vitu vingi, picha za ukweli, mambo haya kule tulipotoka hamna. Lazima uelewe hii ni dunia nyingine,” alisema Papii Kocha wakati wa photoshoot.

Kwa kujiamini, Papii amesema kuwa kazi zao mpya zitakuwa kali zaidi ya zile za zamani. “Kwasababu tumejipanga vizuri na kazi zinazokuja zitakuwa nzuri zaidi ya zile tulizofanya mwanzo,” amesisitiza Papii.

Kwenye photoshoot hiyo iliyofanywa na mpiga picha mahiri Eric Luga, Babu Seya na Papii Kocha walivalishwa na mbunifu wa mavazi, Mtani Nyamakababi.

NEW VIDEO | Engine - Ulingo | Watch


NEW VIDEO | Safi Madiba Ft. Rayvanny - Fine | Watch

6 Jan 2018

NINI NA NAY WA MITEGO WAJIBIZANA KIMAHABA


Rapa na muanzilishi wa lebo ya Free Nation kutoka Tanzania, Nay Wa Mitego ameufungua mwaka kwa ngoma ya mahaba aliyoshirikishwa na Mrembo Mwimbaji kutoka Tanzania ‘Nini’ ambaye walishasemekana kuwa wanatokana kimapenzi.

Ngoma hiyo inayokwenda kwa jina ‘Niwe Dawa’ iliyotayarishwa chni ya Studio za ‘Free Nation’ kwa mkono wa Producer Awesome, mrembo Nini anasikika akimbembeleza na kumhakikishia Nay kwa maneno ya  huba ambayo pia yanayoweza kuwatambulisha kama wapenzi.

“Ukitaka kulala, nami nilale twende ndotoni” Kwa Sauti inyoweza kumtoa nyoka Pangoni” Ni uandishi wa Nini anasikika akiimba.

Kisha Nay naye kwa sauti ya kiume iliyopondeka kwa maneno matamu inajibu juu ya hali zote zilizoelezwa na Nini ambapo kwa ufupi tu Nay anampa Sifa, Bila shaka ni sifa kwa nini kwa mstari unosema  “Napenda unavyoshika Mic, na unavyocontrol Show” ni uandishi wa Nay anasikika akichana.

Video ya ngoma hii imekuwa sana na muonekanao wa kupendeza na iliyosafi kwani kuna muonekano mmoja wa Nay ambao umewakilishwa na Suti matata ya rangi nyeupe ikiwa kazi nima imeongozwa na kuandaliwa na Director Deo Abel ambaye kwa wale wasio mfahamu zaidi ni kuwa ameshirikipia kuandaa na kuongoza video wa wimbo wa Prince Dully Sykes ‘Bombadier’.

Diamond atangaza ujio wa Wasafi FM na Wasafi TV


Rais wa WCB, Diamond Platnumz ametangaza habari njema kwa watanzania hasa hasa kwa wadau wa tasnia ya habari kwamba anatarajia kufungua Wasafi FM na Wasafi TV.

Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo ‘Waka’ akiwa amemshirikisha msanii wa muziki wa kufoka kutoka Marekani, Rick Ross, alitoa taarifa ya ujio wa redio hiyo na TV kupitia twitter yake Disemba 30 mwaka 2017 lakini muda mfupi baadae aliifuta taarifa hiyo.



Weekend iliyopita muimbaji huyo akiwa nchini Kenya katika show za kuufungua mwaka 2018 alifanya mahojiano na kituo cha runinga cha KTN na kueleza mpango wake huo wa kufungua Wasafi FM na Wasafi TV.



Hiyo ni habari njema kwa wadau wa habari kwani kuanzisha kwa kituo hicho bila shaka kitazalisha ajira za kutosha kwa watanzania.

NEW VIDEO | Sam Wa Ukweli – Milele | Watch

NEW VIDEO | Otile Brown Ft. Shettah - Tamu Sana | Watch

NEW VIDEO | BRIDGE Ft. F DAH PRINCE - NAHISI | Watch

NEW VIDEO | Lava Lava - Teja | Watch

1 Jan 2018

T-Pain aitaja albamu bora mwaka 2017


Msanii T-Pain ameitaja albamu yake bora kwa mwaka 2017.

Akiongea na mtandao wa Rap Up msanii huyo ameitaja albamu hiyo kuwa ni Heartbreak on a Full Moon ya Chris Brown yenye ngoma 45 ndani yake.



My favorite album of 2017 would probably be Heartbreak on a Full Moon. For sure. Chris Brown, definitely, guaranteed. There’s enough to pick from. You’re gonna like most of that album, but even if you don’t like most of the album, you’re gonna like an album’s worth of that album,” T-Pain ameuambia mtandao huo.

“There’s for sure 12 songs on there that you’ll like. You can’t go wrong. You cannot not like a big chunk of 45 songs. You’re gonna like an album’s worth of it so there’s no way to lose on that album. There’s no way to not like that album,” ameongeza.

Chris Brown aliachia albamu yake hiyo ya nane October 31 ya mwaka jana.

NEW AUDIO I KIVI CLASSIC - MAUMIVU I DOWNLOAD


NEW AUDIO I J KATA - NI WEWE I DOWNLOAD


Manchester City wapata pigo


Mshambuliaji machachari wa Manchester City, Gabriel Jesus atakuwa nje ya uwanja kwa zaidi ya mwezi mmoja kutokana na jeraha alilopata wakati wa mechi dhidi ya Crystal Palace Jumapili ambapo walitoka sare 0-0, meneja Pep Guardiola amethibitisha hilo.

Mbrazil huyo wa miaka 20 alionekana kuumia kwenye goti kipindi cha kwanza wakati wa mechi hiyo uwanjani Selhurst Park.

Aliondolewa uwanjani akitokwa na machozi.

Kiungo wao Kevin de Bruyne pia huenda akakosa kuwachezea kwa muda baada ya kuondoka uwanjani akiwa amebebwa kwa machela.

Mbelgiji huyo hata hivyo alionekana nje ya uwanja baada ya mechi, dalili kwamba huenda hakuumia sana.

“Nafikiri Gabriel atakuwa nje kwa mwezi mmoja hivi au siku chache zaidi, naye Kevin tutasubiri Jumatatu tujue iwapo aligongwa tu kidogo au ameumia sana,” alisema Guardiola.

Msimamo wa ligi ya EPL 2017/18
Guardiola: Manchester City hawatamaliza ligi bila kushindwa
“Ni lazima ukubali ukali na ugumu wa ukabaji Ligi ya Premia, lakini waamuzi wanahitaji kuwalinda wachezaji, hilo ndilo naomba pekee.”

Jesus atakosa mechi dhidi ya Watford Jumane.

De Bruyne naye ambaye ameng’aa sana msimu huu na kusaidia ufungaji wa mabao tisa Ligi ya Premia msimu huu aliumia baada ya kukabiliwa na kiungo wa Palace, Jason Puncheon.

Barakah The Prince aeleza kilichomfanya avurunde mwaka 2017

Msanii wa muziki, Baraka The Prince amefunguka kueleza kilichomfanya ashindwe kufanya vizuri kimuziki mwaka 2017.
Muimbaji huyo ambaye mwaka 2017 aliachana na label ya Rock Star4000 na kuanzisha label yake, Bana Music, amedai sababu iliyomfanya ashindwe kufanya vizuri ni kukataa baadhi ya show ambazo alikuwa anapewa na mapromota.
“Mi nimiongoni mwa wasanii ambao nabagua sana show, mpaka nikifanya show mpaka promota afike bando ambalo nahitaji, na ninafaya hivyo ili kulinda brand yangu ambayo tayari nimeshaitengeneza,” Baraka alikiambia kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio.

Aliongeza,”Na kama nimeyumba kimaisha nayumba kweli kwa sababu maisha ndivyo yalivyo, kuna kupanda na kushuka, mpaka mataifa mkubwa wanayumba kiuchumi mimi ni nani, sio kitu kibaya, kinaweza kumtokea mtu yeyote”,

Hivi karibuni kumekuwa na malalamiko kutoka kwa maashabiki kuwa msanii huyo sio tu amefulia, bali hata uwezo wake kwenye kazi umeshuka, na kushauri kama inawezekana awe anaandikiwa kazi zake.

Mwaka 2017 ulikuwa mbaya kwangu – Nay wa Mitego


Msanii wa muziki wa Hip Hop, Nay wa Mitego amefunguka kwa kudai kwamba mwaka 2017 uliomalizika weekend iliyopita haukuwa mzuri katika muziki wake.

Rapa huyo ambaye haishiwi matukio, mwaka 2017 aliwekwa ndani na jeshi la polisi kutokana na kuachia wimbo ‘Wapo’ambayo ulidaiwa kuwa maneno ya kutengeneza chuki kwa wananchi na viongozi wao.

“Mwaka 2017 haukua mzuri sanaa. But niseme asante kwa pumzi na afya njema,” aliandika Nay wa Mitego Instagram.


Aliongeza, “Asante mungu kwa Kila Kitu. Asanteni mashabiki wangu ambao mmekua bega kwa bega na mimi kwenye kila jambo ata nilipo kosea hamjawai nitupa, Nawapenda sana. Shukrani kwa media zote kwa support mnayozidi kunipa mungu azidi kuwaongezea mwaka 2018. Happy New Year🔥#NiweDawa,”

Rapa huyo anajipanga kuachia wimbo mpya uitwao, Niwe Dawa.