Artist from Tanzania II Best perfomer II Song Writter II G.LOVE TANZANIA ENTERTAINMENT Dar es Salaam Tanzania Mobile:0766065169 Email.ggodyan@gmail.com.
burudan
https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/
23 Apr 2020
1 Apr 2019
22 Mac 2019
12 Des 2018
4 Des 2018
Gigy Money afunguka “Bora kufanya kazi na Diamond kuliko Alikiba, alinitenga Kahama”

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Gigy Money amefunguka mwanzo mwisho kuhusu kufanya kazi na wasanii wawili wakubwa nchini.
Msanii huyo amefunguka kuhusu kufanya kazi na Diamond pia na Alikiba na kusema kuwa “Alikiba anakunja sana kuliko Diamond na siku wameenda kufanya wote show Kahama, Alikiba alimtenga back stage”
Tigo Fiesta kufanyika Dar mwaka huu , yaja na surprise za kutosha

Uongozi wa Clouds Media Group, umetangaza kuwa tamasha la Fiesta ambalo liliahirishwa kufanyika Dar Es Salaam mwishoni mwa mwezi Oktoba, litarudiwa tena mwezi huu.
Taarifa hizo za kurudiwa kwa tamasha hilo, zimethibitishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media, Joseph Kusaga kupitia kipindi cha Clouds 360.
Kwa upande mwingine, bado haijaelezwa ni sehemu gani tamasha hilo litafanyika? na kiingilio kitakuwa ni shilingi ngapi?.
Tarehe 24 Oktoba mwaka huu, ni siku ambayo tamasha la Tigo Fiesta lilipangwa kufanyika, lakini baadae liliahirishwa kwa amri ya Serikali ya Manispaa ya Kinondoni.
4 Nov 2018
29 Jul 2018
Hii ndio show kali zaidi ya Diamond Platnumz kuwahi kutokea, awaimbisha kiswahili Wafaransa kisiwani Mayotte
Kwa sasa ukitaja majina ya wasanii 10 bora wanaofanya vizuri barani Afrika huwezi kuacha kumtaja Diamond Platnumz hii ni kutokana na kuongezeka kwa wigo mpana wa mashabiki wake.
Hili la kuongezeka kwa idadai ya mashabiki linajidhihirisha hata pale Diamond anapokuwa nje ya Tanzania hususani katika mataifa ambayo hayaongei Kiswahili.
Jana Julai 28, 2018 Diamond Platnumz alikuwa katika visiwa vya Mayotte nchini Ufaransa ambapo aliweza kutumbuiza nyimbo zake zote tena zile ambazo hajafanya kolabo na jambo la kufurahisha licha ya asilimia 99% ya wananc
7 Jun 2018
Muziki wa Diamond unakosha roho hata kwa sisi wazee – Mrema
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole, Augustino Mrema amesema msanii wa Bongo Flava anayemfuatilia kwa sana ni Diamond Platnumz.
Ameeleza sababu ya kumfuatilia muimbaji huyo ni kutokana na kujituma kwake na muziki wake unavutia.
“Namfuatilia sana Diamond, ni kijana mdogo, muimbaji mahiri, yaani Diamond asaidiwe naona hatima yake katika maisha yake na nchi yetu atatufikisha mahali pazuri. Kwa muziki wake unakosha roho, hata sisi wazee, mimi naridhika sana,” Mrema ameiambia Times FM.
Katika hatua nyingine ametoa wito kwa serikali kuwa karibu zaidi na wasanii, hata hivyo amesema anaziona jitihada za Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe za kukutana na wasanii kila mara hasa pale wanapopata matatizo na kuwasaidia.
Madee huwa simuelewi, anatoa biti sio wimbo tena – Belle 9
Msanii Belle 9 amesema moja ya wasanii asiyowaelewa katika Bongo Flava ni Madee.
Muimbaji huyo akipiga stori na JJ wa Jembe FM amesema kuwa kutokana anasikiliza wachanaji wengi wanaofanya vizuri anahisi kuna kitu anakikosa kutoka kwa Madee.
“Honesty, let me be honesty, Madee huwa simuelewi. I don’t know, ujue kuna wasanii inafika kipindi unasikiliza unasema huyo mtu ana-release beat sio wimbo tena,” amesema.
“Labda kwa vile nasikiliza rappers ambao wanajua sana au kuna kitu nakitegemea kutoka kwake kutokana muda mrefu yupo kwenye game, kuna kitu nakimisi, so naona kama nikimsiliza na lose,” amesisiza.
Belle 9 ambaye anafanya vizuri na ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la Dada, ameongeza kuwa mara nyingi ni vigumu mtu anayetoa kauli kama yake kueleweka ila yeye amesema kile ambacho anaona kipo sawa na kuwataka mashabiki wa Madee kuchukulia kawaida.
31 Mei 2018
30 Mei 2018
Baada ya kupata kigugumizi cha ndoa, Rayvanny anyoosha maneno
Baada ya Rayvanny kupata kigugumizi kuhusu kufunga ndoa na mpenzi wake Fahyma, sasa ameweka mambo wazi.
“Yeah, Mungu akijalia lakini kwa sasa siwezi kusema ni lini kwa sababu hivi vitu vinapangwa na familia, ndugu mkishapanga. ikishakuwa official kila mtu atajua,” alisema Rayvanny hivi karibuni kwenye uzinduzi wa filamu ya Aunty Ezekiel, Mama.
Habari njema kwa sasa, hit maker huyo wa Pochi Nene kupitia mtandao wa Instagram ameweka wazi kuwa ndoa yake itafanyika hivi karibuni tena na mama watoto wake Fahyma.
“🌸 @fahyvanny NDOA SOOOOOON can’t Wait,” ameandika Ray kwenye mtandao huo.
G Nako amtabiria makubwa Vanessa Mdee
Msanii wa muziki Bongo kutoka kundi la Weusi, G Nako amesema kolabo yake na Vanessa Mdee ‘Wet’ itafika mbali zaidi ya sasa.
Wakati G Nako akipiga stori na JJ wa Jembe FM amesema kuwa wimbo huo toka wakiurekodi walijua utakuja kufika mbali.
“Ni wimbo nzuri toka tulivyoureekodi, wakati albamu bado inaendelea kutengenezwa ilionyesha ni moja ya nyimbo zitakuja kufanya vizuri kwenye albamu,” amesema.
“So nafikiri mafanikio bado yataendelea kuwa makubwa na tunasubiri mafanikio mengine makubwa zaidi na mimi bado nashukuru kwa watu wote ambao wanaendelea ku-support,” amesisitiza.
Wet ni miongoni mwa nyimbo ambazo zimetoka rasmi pamoja na video zake kutoka kwenye albamu ya kwanza ya Vanessa Mdee inayokwenda kwa jina la Money Mondays.
Kati ya Rihanna, Wizkid na Yemi Alade, mmoja wapo ana kolabo na Nandy
Msanii wa muziki Bongo, Nandy ametaja orodha ya wasanii wa kimataifa ambao anatamani kufanya nao kazi.
Muimbaji huyo anayetamba na ngoma ‘Ninogeshe’ amewataja wasanii hao kuwa ni Rihanna, Wizkid na Yeme Alade, huku akiweka wazi kuwa kazi na Yemi Alade ipo tayari.
“Wapo kama watatu Yeme Alade, kuna Wizkid and Rihanna, kila mtu ana wish, ipo kazi kwa mmoja; Yeme Alade,” Nandy ameiambia Hot90 Fm.
Katika hatua nyingine Nandy amesema kuwa katika maisha yake ya kimahusiano angetamani kujaliwa kupata watoto mapacha.
Diamond anafanya kazi, sijui hata kama huwa analala – Master J
Producer Mkongwe wa muziki Bongo, Master J amesema kuwa mafanikio ya Diamond Platnumz katika muziki ni kutokana na juhudi zake.
Master J amesema ambao wanaweza kumshangaa mafanikio anayopata kwa sasa pengine ni wale waliomjua hivi karibuni.
“Kwa wale ambao wanamjua kwa undani wanajua kwamba hivi vitu havijaja kwa urahisi, ni mtu ambaye anafanya kazi, sijui hata kama huwa analala, ana juhudi na ana bidii sana, kwa hiyo haya matunda tunaona leo ni matokeo kujitoa kwa miaka mingi sana,” amesema.
“Kwa hiyo mimi ninavyoona sasa hivi anaanza kupata matunda kusema kweli nafurahi sana na ninamshukuru Mungu,” Master J ameiambia Wasafi TV.
Licha ya kufanya vizuri katika muziki wa Bongo Flava, Diamond ameingiza bidhaa zake sokoni ‘Chibu Perfume na Diamond Karanga’ na sasa amefungua Wasafi Media na hivi majuzi ameweka wazi kumiliki moja gari la kifahari.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)








