burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

1 Nov 2017

Baada ya Jux, Vanessa Mdee atua kwa Cassper Nyovest


Msanii wa muziki wa Bongo Flava, Vanessa Mdee amezidi kuonyesha uwezo wake kwa upande wa ‘video queen’ mara baada ya kuonekana katika video ya rapper Cassper Nyovest kutoka nchini Afrika Kusini.

Hii si mara kwanza kwa Vanessa kufanya hivyo, utakumbuka January 2015 alitokea kwenye video ya Jux katika ngoma ‘Sisikii’, baada ya hapo waliweza kutoka ngoma ya pamoja inayokwenda kwa jina la Juu.

Hata hivyo kuna uwezekana mkubwa Cassper Nyovest akapita katika nyayo za Jux kwa kuja kuachia ngoma na Vanessa. Akizungumza na Dj Show ya Radio One Vanessa amesema kuna muendelezo wa kazi kati yake na rapper huyo.

“Ni project endelevu tumeanza kwanza na video yake ya ‘Baby Girl’ ambayo nimecheza, so next msubirie kidogo itakuja very soon” amesema Vanessa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni