burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

30 Mac 2017

Hii ndio sababu ya show ya Drake ya Amsterdam kuvunjika


Drake alilazimika kuivunja show yake ya mjini Amsterdam Jumatatu hii baada ya kudaiwa kuugua ghafla. Kumbe rapper huyo alikula chakula chenye sumu!

Mtu wa karibu wa rapper huyo ameuambia mtandao wa TMZ kuwa rapper huyo alikula chakula hicho chenye sumu muda mfupi kabla ya kufanyika kwa show hiyo.

Drake alikimbizwa hospitali ndipo madaktari walipomshahauri kutofanya show hiyo. Mashabiki walimsubiri rapper huyo katika ukumbi wa Ziggo Dome kwaajili ya kutumbuiza kwa muda wa dakika 75 kabla ya kutangaziwa kuvunjika kwa show hiyo.

Hata hivyo show hiyo inatarajiwa kufanyika tena Jumatano hii katka ukumbi huo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni