burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

3 Jul 2017

Siumizi kichwa kuandaa hit song – Z Anto


Msanii wa muziki, Z Anto amefunguka kwa kudai kuwa katika maisha yake ya muziki hajawahi kupata shinda katika kuandaa hit song.

Muimbaji huyo ambaye amekaa kimya kwa muda mrefu bila kuacha kazi, ameiambia Bongo5 kuwa ukimya wake haujasababishwa na ugumu wa game ya muziki bali alikuwa anafanya biashara zake nyingine.

“Kusema kweli mimi ni msanii ambaye nikiamua kuandaa hit song naandaa mara moja tu, tena hit song huwa naziandaa kama nikiwa nje ya muziki wa muda fulani hata ukiangalia wimbo Binti Kiziwi nilikaa muda lakini baada ya kurudi nikaja kufanya maajabu,” alisema Z Anto.

Anto amedai ukimya wake ulitokana na kufanya mambo yake binafsi nje ya muziki.

Muimbaji huyo amedai kwasasa haoni kama kuna changamoto kwa msanii kufanya vizuri kama msanii akiamua kufanya muziki mzuri.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni