burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

21 Sep 2017

Adui wa mwanamke ni mwanamke mwenzie – Shamfa Ford


Wakati moto ukiendelea kuwaka Hamisa Mobetto kujulikana kuzaaDiamond Platnumz wakati akiwa na mhusiano na mpenzi wake Zari. Msanii wa filamu Bongo, Shamsa Ford amefunguka na kuwafunda wanawake kwa kusema kuwa adui wa mwanamke ni mwanamke mwenzie.

Shamsa Ford ambaye ni mke wa halali wa Chid Mapenzi, mashabiki wameibua mzozo katika mtandao wa Instagram ambao baadhi ya mashabiki wamedai kuwa anamuonea wivu Hamisa.

Adui wa mwanamke ni mwanamke mwenzie.haitakuja kutokea kamwe wanawake tukapendana.mwanamke ndo huwa mstari wa mbele kumuumiza na kumdhalilisha mwanamke mwenzie.kabla ya kumuumiza mwanamke mwenzio jaribu kuvaa viatu vyake ingekuwa wewe ungefanyaje..wanawake sisi daaa####TUNAHITAJI MAOMBI

Shamsa amekuwa akiutumia ukurasa wake wa instagram kuwandika mambo mbalimbali ya kushauri wanawake na watu ambao bado hawajaingia kwenye ndoa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni