burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

3 Sep 2017

B Dozen atia neno mvutano wa Diamond na Alikiba, ‘ni kitu kizuri’


Host wa show ya XXL ya Clouds Fm, B Dozen amefunguka mambo machache kuhusu mvutano wa Diamond na Alikiba pamoja na team zao katika mitandao ya kijamii.

Katika mahojiano na Times Fm kwenye kwenye uzinduzi wa viatu ‘SultanXforemen’ vya msanii wa filamu na mchekeshaji, Idris Sultan. B Dozen alisema ni kitu kizuri iwapo kitawaletea fedha.

“Ni game inasonga mbele, unaona kama kwenye wiki hizi mbili pamechangamka kweli, kumekuwa na team hii na team hii as long as hakuna ambacho kitatokea baada ya mabishano yanayondelea kwenye social media, radio station na Tv kwenye interview zao,” amesema.

“Ni kitu kizuri ilimradi kiwe kinawatengenezea hela isiwe ni tuwe na namba kubwa ya followers na like kwenye page zao na views kwenye YouTube bila ku-make money it won’t make sense lakini kama inatengeneza hela it very goog thing,” ameongeza.

Siku za hivi karibuni Diamond na Alikiba pamoja na mashabiki wao walikuwa na mchuano mkali katika mitandao ya kijamiii baaada ya kutoka ngoma ‘Seduce Me’ ya Alikiba na ‘Zilipendwa’ ya Diamond/WCB.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni