burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

4 Okt 2016

Barnaba: Nimeshauza maji, nshafanya kazi kwa mamantilie, nshaitiwa mwizi…

14574163_1654664108179037_5724717438747017216_n
Anaweza kuwa mmoja wa wanamuziki wa Bongo Flava waliofanikiwa kwa kiasi kikubwa kwa sasa, lakini Barnaba amepitia mengi. Ameshawahi kufanya karibu kila kazi unayoweza kuifikiria.
“Kabla ya kuanza huu muziki nishauza maji, nshauza mamantilie, nishakuwa fundi makenika,” Barnaba alikiambia kipindi cha The Playlist cha Times kinachoendeshwa na Lil Ommy hivi karibuni.
“Nishaitiwa mwizi, nshauza siso, nshauza vyuma, nshakuwa fundi umeme, nshakuwa fundi nyumba,” aliongeza.
Alidai kuwa kuna wakati alikuwa akilala kwenye makuti katika kibanda kilichokuwa nje ya studio ya dada aitwaye Nzela baada ya kufukuzwa THT.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni