burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

30 Nov 2016

Nick wa Pili akerwa na mashabiki kwenye muziki

Rapper Nick wa Pili amedai kuwa anachukia kuona mashabiki wakibishana kuhusiana na mambo yasiyo na faida kwenye muziki.
15056643_240347599718846_3937226945791524864_n
Akiongea na kipindi cha Ladha 3600 cha EFM Jumanne hii, hitmaker huyo wa Sweet Mangi amesema kuwa anafurahi akiona mashabiki wakibishana kuhusu muziki na ubunifu wa wasanii kwenye muziki wao.
“Mimi sikatai mashabiki kubishana ila wabishane kuhusu muziki sio nani kakaa wapi anafanya nini. Ningefurahi kama wangebishana kuhusu show, ubunifu,” amesema.
“Unapoona mtu amesema fulani namba moja huna haja ya ‘Kudebate’ hii inatokana na maoni vile ambavyo mtu anaona na anapima kwa vigezo vyake. Msanii wa Hip Hop anapokuwa na top track sote tunapaswa kufurahia,” ameongeza.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni