burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

26 Nov 2016

Ommy Dimpoz: Nilichangia kuandika Nasema Nawe ya Diamond

Ommy Dimpoz amesema alichangia kuandika hit single ya Diamond, Nasema Nawe – kipindi bado ni marafiki.
“Mimi nataka kusema kitu kimoja, sijawahi kusema sehemu yoyote hapa, mfano kwenye nyimbo ya mduara ya D Nasema Nawe, mimi nimechangia kwa asilimia kubwwa uandishi wa ile nyimbo. Sio kwamba D hajui kuandika, anaandika vizuri na nawaheshimu ni moja ya waandishi bora kabisa,” Ommy alikiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM, Alhamis hii.
Ametolea mfano mstari aliochangia ni wa verse ya pili usemao ‘zingifuli zingifuli usozinga mahala ukakaa.’ Muimbaji huyo amesema hata kwenye verse ya kwanza kuna maneno ameyaandika lakini hakuwahi kutaka apewe credit.
“Sikufanya vile kwasababu nilipwe au nipewe credit. Lakini nataka tu niseme kuwa mashabiki kuna vitu vingine vingi hawajui,” alisisitiza.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni