burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

7 Okt 2016

Vanessa Mdee aipiga chini show ya Chris Brown Mombasa

Ndoto ya Vanessa Mdee kutumbuiza kwenye jukwaa moja na msanii wa Marekani, Chris Brown kwenye tamasha la Mombasa Rocks Music Jumamosi hii imepeperuka.
14448268_1797915360467373_2150686740120076288_n
Hitmaker huyo wa ‘Niroge’ ameweka wazi kupitia mtandao wake wa Instagram sababu ya kutotumbuiza kwenye tamasha hilo ni kutofikia makubaliano na waandaaji wa tamasha hilo.
14478527_1592720981023421_8041592067165519872_n
Kwa sasa macho ya Vanessa yatakuwa ni kwenye tamasha la One Africa Music litakalofanyika jijini Houston, Texas, Marekani, October 22 ambapo anatarajiwa kupanda kwenye jukwaa moja na wasanii wengine kama 2 Face, Flavour, P –Square, D’Banj, Kcee, Mafikizolo, Fally Ipupa na Cabo Snoop.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni