burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

31 Jan 2017

Aunt Ezekiel adai matendo machafu ya wasanii yamechangia kuporomoka kwa soko la filamu


Msanii wa filamu na mama wa mtoto mmoja Aunt Ezekel amedai matendo machafu ya wasanii wa filamu ni moja kati ya vitu ambavyo zimechangia kushuka kwa soko la filamu nchini.

Muigizaji huyo ambaye kwa sasa yuko kwenye mahusiano ya kudumu na dansa wa WCB, Mose Iyobo amedai wasanii wengi wa filamu wameendekeza starehe kuliko kasi.

“Kipindi hiki filamu zimepoteza mvuto na watu wamekuwa wakizungumza mengi ila ninachoona mimi ni matendo yetu machafu yanachangia,” Aunt aliliambia gazeti la Mtanzania. “Mbona wasanii kama kina King Majuto bado wanafanya vizuri? Skendo zinayumbisha soko la filamu na siyo kitu kingine,”

Kati ya skendo ambazo zinatajwa zaidi kuwatikisa wasanii wa kike wa filamu ni kutoka na waumume wa watu, kuolewa na kuachika pamoja na kubadilisha mabwana mara kwa mara.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni