burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

31 Jan 2017

Hii ndio tarehe ambayo album ya Fid Q ‘Kitaaolojia’ itatoka


Ni mwaka wa tatu sasa tumekuwa tukisubiri album ya tatu ya Fid Q, Kitaaolojia.
Kwanini haitoki, ama nayo inataka kuwa kama Detox ya Dr Dre? Habari njema ni kuwa, album hiyo mwaka huu lazima iingie mtaani ili kusambaza hiyo elimu ya mtaa, iliyobeba jina lake.

“Kitaaolojia ni kweli ina miaka mitatu imekuwa kama Detox na nini, lakini unajua mimi ni perfectionist, natakaa itokee kweli konki,” Fareed ameiambia Bongo5.

“Na idea zimekuwa zikibadilika mara kwa mara, lakini so far sasa hivi nimeshaipatia direction, na kuna uhakika ninaweza nikawaguarantee kabisa kwamba August 13 ya mwaka huu panapo majaliwa Kitaalojia itakuwa mtaani,” amesisitiza.

Fid ameshatoa album mbili hadi sasa, Vina Mwanzo Kati na Mwisho na Propaganda.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni