burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

31 Jan 2017

Belle 9 aelezea umaskini ulivyomfanya mpenzi wake aporwe na mtu aliyekuwa akimfahamu


Wimbo, Sumu ya Penzi uliomtoa Belle 9, ulikuwa ni true story.
Aliuandika baada ya mpenzi wake kummwaga na kuanzisha uhusiano na mtu aliyekuwa akimfahamu.
“Ilinichukua muda sana kuzoea ile hali,” Belle 9 alisema kwenye mahojiano na Lil Ommy kwenye kipindi cha The Playlist cha Times FM.

“Kwasababu kitu ambacho kilichokuwa kinaniuma ilikuwa katoka kwangu halafu kaenda kwa mtu ambaye namfahamu kabisa, na yule mtu maisha ya kwao na maisha ya nyumbani ni tofauti. Yule alikuwa hata siku tukienda kwenye mpira kila siku anabadilisha six, anabadilisha jezi, sisi ndio tulikuwa wale watu ambao tunarudia hizo hizo kila siku,” aliongeza.

“So akawa anapita naye maskani ambapo sisi tunakaa sababu yeye alikuwa anakaa mtaa wa juu, sasa kuna barabara pale nyumbani ilikuwa inapita kwenda chini kuna ukumbi fulani ambao ndio tulikuwa tunaimbaimba, kuna kama karestaurant fulani, so wakawa wanapita maskani pale wanaenda kule, wameshikana mkono, wameshikana viuno, halafu mchizi anasimama anasalimia sasa, ni kitu ambacho kiliniuma sana.”

Belle amedai kuwa hadi sasa msichana huyo anajutia kitendo alichomfanyia.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni