burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

21 Jan 2017

Black Rhyno kumshtaki Nay wa Mitego kisa beat? Sikia alichokisema

Kwenye playlist ya ngoma kali zilizotoka mwaka jana mwishoni, haziwezi kukosa sijiwezi ya Nay wa Mitego na Kama Movie ya Black Rhyno aliyompa shavu Jux.

Ngoma hizi zimezua utata kwani ni ngoma ambazo zina beat moja na zote zimetengenezwa na producer Mr T Touch.
Nimepiga story na Black Rhyno kwenye show yangu ya Supermega kupitia Kings Fm kutaka kufahamu kama atamshtaki Nay kwani ana haki miliki ya mdundo huo.
“Kuamua kumshtaki ni maamuzi yangu..mimi bado sijaamua kumshtaki,ila nikiamua kumshtaki basi nitamshtaki na itajulikana watu wote mtajua kama nimemshtaki,”amesema Black Rhyno.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni