burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

21 Jan 2017

Ommy Dimpoz aeleza kwanini alisita kuingiza sokoni mavazi ya PKP


Kuna wakati Ommy Dimpoz aliwahi kuahidi kuwa angeingiza sokoni mavazi ya brand yake ya PKP na aliwahi kutengeneza hadi sample zake.
Lakini hadi sasa, hakuna dalili kuwa mavazi hayo yatazinduliwa rasmi.

Akiongea na Bongo5, Ommy amesema alisita kuingia kichwa kichwa kwenye biashara hiyo sababu aligundua atawanufaisha wajanja wachache.



“Kama kwa biashara ya kutaka sifa nionekane na brand ya vitu vyangu, sawa, lakini kama kwaajili ya kutengeneza pesa hii bado ni ngumu sababu ni kama unawafanyia promotion watu wengine,” amesema.

Ommy anadai kuwa kuna wafanyabiashara kibao ambao wanasubiri mastaa waanzishe brand zao na kisha kwao kwenda kutengeneza makontena ya mzigo China na kuuza kwa bei nafuu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni