burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

13 Jan 2017

Darassa kuja na album yake mwaka huu, aeleza itakavyokuwa

Image result for darasa
Darassa amesema anatarajia kuachia album yake mwaka huu. Akiongea kwenye kipindi cha Ladha 3600 cha EFM, hitmaker huyo wa Muziki amedai kuwa yeye na uongozi wake wanalifanyia kazi suala hilo ili kuhakikisha anawapa mashabiki wake muziki wa aina mbalimbali.

“Nafikiri before mwaka kuisha tutakuwa na album sasa ambayo kwa kurahisisha kupata muziki wote ambao watu wetu wanauhitaji sababu still Darassa ni yule yule,” amesema.

“Ukisikiliza nyimbo kama Sikati Tamaa unakuta spirit ndio kitu kinachotembea mle ndani kwenye Muziki unakuta ni spirit ndio kitu kinachotembea mle ndani so tunabadilika kutokana na hali halisi na dunia inavyomove. Hatuwezi kusema tunabaki kule kule wakati dunia imeenda 2017, hatuwezi kuwajenga watu ambao wanakuja, hatuwezi kujenga taifa ambalo linakuja, hatuwezi kujenga taifa ambalo linakuwa na maana ya dunia ya leo, lazima tukubali mabadiliko.”

Kwa upande mwingine Darassa amesema hana wasiwasi na nguvu ya Muziki ilivyo kwa sasa katika kuja na wimbo mwingine utakaoweza kumwendeleza mbele ya alipofikia. Amedai kuwa yeye na uongozi wake wapo tayari kwa lolote.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni