burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

13 Jan 2017

Seline atoa povu kwa wasanii wa kike Bongo


Msanii wa kike aliyewahi kuwa chini ya usimamizi wa label ya The Industry iliyo chini ya kundi la Navy Kenzo linaloundwa na wasanii Aika na Nahreel, Seline amefunguka kuhusiana na wasanii wa kike kutumia skendo kwa kujiongezea umaarufu.
Akizungumza na Mtangazaji Pk5tz wa kipindi cha Extra Fleva cha Uplands FM ya Njombe, Seline ambaye sasa yupo chini ya usimamizi wa Producer Mona Gangstar wa Classic Sound, amesema kitu anachokichukia kwa sasa ni wasanii wa kike kutumia skendo kwa ajili ya kupromote kazi zao.

Seline amedai wakati mwingine ni nzuri sababu zinamfanya msanii azungumziwe ingawa wakati mwingine ni vyema msanii akaamini katika kipaji alichonacho kwakuwa skendo zina changamoto yake.

Kwa upande mwingine, akizungumzia kuhusu uzoefu wa kuwa chini ya label, Seline amewatupia lawama wasimamzi wanaosimamia wasanii bila kuwa taaluma na hiyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni