burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

31 Jan 2017

Napenda kufanya kazi nje ya matarajio ya wengi – Joh Makini

Joh Makini anataka kuweka kitu kimoja ‘very clear’ kuwa hupenda kufanya kazi nje ya matarajio ya wengi.
Kauli yake inakuwa jibu kwa baadhi ya mashabiki walio na mtazamo tofauti na kazi yake mpya, Waya.
“Siku zote kwenye sanaa, lazima uwe mtu tofauti na usiyetabirika kwamba unakuja vipi,” Joh alimuambia mtangazaji, Eddy Msafi kupitia kipindi cha Full Charge cha Pride FM ya Mtwara.
“Kwa maana hiyo nimeona Waya ni wimbo mzuri na mkali na unaweza kufanya vizuri sehemu yoyote duniani na utakuwa ni msimu mzuri ukitoka wakati watu wanaelekea Valentine’s,” ameongeza.

Joh hakusita pia kukumbusha kuwa Waya kwa sasa ndio video inayotrend katika nafasi ya kwanza kwenye mtandao wa Youtube.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni