burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

31 Jan 2017

Baba na mama yangu ndio couple ninayoikubali zaidi – Belle 9

Ni couple gani ambayo unailewa zaidi hapa Bongo? Ni swali ambalo mtangazaji wa kipindi cha The Playlist cha Times FM, Lil Ommy alimuuliza Belle 9.
“Wananivutia kwasababu nyumbani maisha ni ya kawaida lakini still baba yuko na mama halafu mara zote ambazo nimekuwa nyumbani, sijawahi kuona mama yangu anagombana na baba. Mimi nimekaa sana nyumbani kwa muda mrefu, lakini mara ya kwanza naona kama wanashikanashikana hivi ilikuwa mimi ndio chanzo, yaani mama alikuwa ananitetea mimi kwasababu baba alikuwa ananinyoosha sana sasa mama alikuwa kama anaingia hivi, lakini haukuwa ugomvi,” ameongeza.
“Kiukwezi ni best couple kwangu mimi, najifunza mengi kupitia pale, inanipa nguvu nikirudi nyumbani baba yupo, mama yupo nikitoka hapo nami nakuwa nipo fast kila kitu.”

Kwa upande wa couple ambayo haielewi ni ile ya Kanye West na Kim Kardashian.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni