burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

9 Mei 2017

STEVEN SEAGAL APIGWA MARUFUKU KUKANYAGA UKRAINE, ATANGAZWA TISHIO KWA USALAMA WA NCHI


Muigizaji mkongwe wa filamu za kipigo, Steven Seagal amepigwa marufuku kukanyaga ardhi ya Ukraine, lakini pia kutangazwa kuwa ni tishio kwa usalama wa nchi hiyo.

Taarifa kutoka nchini humo zimedai kuwa mamlaka za usalama zimechapisha barua kutangaza kuwa Seagal hatakiwi kuingia nchini humo kwa miaka mitano ijayo.



Kwa mujibu wa barua hiyo, Seagal amefanya vitendo vya hatari kijamii ambavyo vinaingiliana na nia ya kulinda usalama wa Ukraine. Kosa la Seagal ni kuonekana akiwa pamoja na watu watata wakiwemo Alexander Lukashenko na Rais wa Urusi, Vladimir Putin.

Sababu nyingine ni muigizaji huyo kupewa uraia wa Urusi na Rais Putin.

Urusi na Ukraine zimekuwa kwenye mgogoro wa kisiasa tangia mwaka 2014 na tayari nchi hiyo imewawahi kuwazuia wasanii 140 wa Urusi kuingia.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni