burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

9 Mei 2017

Young Dee aeleza kisa cha kutimka MDB na kujiunga King Cash


Rapa kutoka King Cash, Young Dee amefunguka kueleza kilichosababisha akaondoka katika label yake ya zamani, Millian Dollar Boys (MDB) iliyochini ya producer Max Rioba.

Rapa huyo ambaye ameachia video ya wimbo wake mpya ‘Bongo Bahati Mbaya’ akiwa chini ya label hiyo mpya, ameiambia Bongo5 kuwa aliachana na label hiyo baada ya kushindwa kukubaliana baadhi ya mambo.

“Nikianza na watu ambao nilikuwa nikifanya nao kazi ni watu ambao nilikuwa nafanya nao kazi kama familia,” alisema Young Dee. “So lilivyokuja suala la kifamilia kuna baadhi ya vitu havikwenda sawa ndipo ikaoneka kila mtu aanze kufanya kazi mwenyewe bila kumtegemea mtu mwingine,”

Aliongeza, “Mimi suala la kufanya kazi na Mr Ttouch ni suala la muda hata hapo awali tulikuwa tunafanya kazi kama washkaji. Kwahiyo baada ya kuona tunaweza kufanya kazi pamoja, akanikutanisha na uongozi wa King Cash, wakanisaini kama msanii wao wa kwanza,”

Rapa huyo alisema yeye pamoja na Mr TTouch wapo chini ya King Cash.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni