burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

21 Des 2016

Witness awajibu wanaomsema vibaya kuhusu unene wake


Rapper wa kike Bongo, Witness a.k.a Kibonge Mwepesi amewajia juu watu wanaomsema vibaya kuhusu unene wake.
Witness ameonyesha kuchukizwa na maneno hayo na kuamua kutoa yake ya moyoni kupitia mtandao wa Instagram kwa kusema kuwa watu wanachukia kuona mahusiano yake na mpenzi wake Ochu lakini pia kuhusu unene wake si kweli ila watataka apunguze makalio yake kitu ambacho kwake hakitawezekana

Kupitia mtandao huo, rapper huyo ameandika:

Wakati mwingine watu hawanichukii mimi huchukia namna tunapendana mpenzi wangu @ochusheggy wanasema mineno kibao, roho zinawauma mpaka wanaona ni heri waanze kuni attack kwa kunitukana na wanaanza kunisakama kwamba oooh! Unauza vitu vya Kupunguza mwili wewe mwenyewe mnene kinachonishangaza ni kwamba nia yao siyo nipunguze mwili Nia yao nipunguze tako langu LA kinyakyusa a.k.a #msambwanda kajisemea kaka @diamondplatnumz sasa basi Nina waahidi nitapungua kote na nimekwisha pungua picha 2017 Ila siyo tako langu LA kinyakyusa sijalinunua dukani nimezaliwa nalo, not chinese not imported, ndo maana sijisumbui kununua wala kuongeza matako feki kama nyie, yasije nitokea puani BURE na nnajua ya kuwa wanajua ya kuwa moja kati ya qualities nilizo nazo hadi mtoto wa kisambaa kabaki ni #msambwanda wangu na nnajua ninao so plz stop wasting ur time kwa kujidai oooh mbona wewe nyong’o nyong’onyong’o nyong’o Kupunguza tako,na sasa kinacho wanyonha ni kwamba nikipunguza tumbo ndo inakuwa balaa shepu yangu ndo inajichora vizuri #figanambanane original not Chinese not imported, mwanamke wa kiafrica ninayejivunia Rangi yangu
.
.
. .
Na kwa taarifa yenu kila mwanaume anapenda aina ya mwanamke wake, wengine wanapenda vimbau mbau haya,wenye kupenda misambwanda haya twende kazi wenye kupenda Wanene kipendacho roho tena but kuna watu kwa kufuatilia ya wenzao utadhani wamezaliwa mlango wa nyuma #kwataarifayenu sintopunguza katu msambwanda wangu sir godi mwenyewe wakati anautengeneza aliamua kwenda lunch Kwanza akirudi ndo aumalizie he he he heheeeeeeee #roshorobibiustakencheke mie! Nisemeni vyote siyo hicho na kwa kifupi siwasikilizi mtalipuka mapepo sana humu Insta na hakunaga wachungajiπŸ˜πŸ˜πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€ #teamzzzzzzzzzzzz!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni