burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

14 Apr 2017

Hii ndio tarehe ya mkutano mkuu wa TFF

Shirikisho la Soka Tanzania TFF, limetangaza kufanya Mkutano wake Mkuu siku ya Jumapili ya Agosti 12, 2017.

Maamuzi hayo yamefanyika katika kikao cha Kamati ya Utendaji cha Shirikisho hilo, kilichokutana siku ya Jumapili Aprili 9, 2017 ambapo miongoni mwa ajenda katika mkutano huo, itakuwa ni uchaguzi mkuu wa TFF.

Kwa mujibu wa Katiba, uchaguzi huo utachagua Rais wa TFF, Makamu Rais wa TFF na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni