burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

26 Apr 2017

Ujio wa Tumbo bandia kuwasaidia watoto Njiti duniani


Wanasayansi kutokea nchini Marekani hatimaye wamebuni tumbo bandia, ambalo linategemewa kuja kutumika kuhifadhia watoto wanaozaliwa kabla ya muda wao (Njiti).

Watafiti katika hospitali ya watoto mjini Philadephia, wanasema kuwa lengo lao ni kuweka mazingira salama kwa watoto wanaozaliwa kabla muda wao kutimia.


Kifaa hicho maalumi chenye muonekano wa tumbo kimejaribiwa kwa kubebea mimba ya kondoo. Kitatumiaka kubebea Njiti iliwanaweza kukuza viungo vyao vya mwilini kama vile mapafu na viungo vyengine.

Wanasayansi wanaamini mfuko huo ama tumbo hilo bandia linaweza kua tayari kwa majaribio ya binadamu kuanzia miaka mitatu mpaka mitano kuanzia sasa. Kifaa hicho kimetengezwa na wanasayansi kwa kutumia mifuko ya plastiki

Takwimu za shirika la afya dunaini zinaonyesha wastani wa watoto milioni 15 huzaliwa njiti ulimwenguni kote.





Kuzaliwa kabla ya muda ni tatizo linalochangia na kusababisha vifo vya watoto wachanga na inakadiriwa kufikia asilimia 27 ya vifo hivyo kwa Tanzania. Vifo hivyo husababishwa na kuzaliwa njiti, magonjwa ya vimelea vya bakteria, matatizo ya kupumua na kuvuja damu.



Hospitali ya Taifa Muhimbili imekuwa mfano katika kutekeleza mpango wa kangaroo wa kusaidia watoto wanaozaliwa njiti.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni