burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

22 Apr 2017

PRODUCER P. FUNK ‘MAJANI’ ATANGAZA UTARATIBU MPYA WA UFANYAJI WAKE WA KAZI.


Jina P. Funk ‘Majani’ ni moja kati ya majina makubwa kwenye ulimwengu wa muziki wa Bongo fleva ambao asili yake ni Tanzania,ukubwa wa jina la Majani linakuja pale ambapo muziki huu ulianza kusikilizwa na kupendwa na watu wengi baada ya mikono yake kuhusika kuzalisha hits nyingi za miaka ya nyuma.

Popote unapolisikia jina la Majani picha inayokuja ni haraka ni muziki mzuri ambao umeendelea kuishi ndani yake mpaka sasa,Majani ameamua kuchukua sekunde kadhaa kuelezea zaidi namna ambavyo amebadilisha utaratibu wa studio yake kwa wale watakaohitaji zaidi kwenda kurekodi au kufanya kazi nae.

Kwenye XXL ya Clouds FM,Majani amesema>>’Wewe unakua umerekodi studio yako nyingine ukitaka sauti uweke kwenye mic za Kimataifa zipitie kwenye mashine za Kimataifa na sikio la Kimataifa unalipa kiasi fulani,ukitaka mixing kama ni studio fulani naweza kwenda kwenye hiyo studio nikachukua hizo files’

‘Nikifanya hivyo haki zote ni zako wewe unanilipa kwa shughuli ya ngu kwa sababu mimi sijaunda huo muziki,lakini hii imekuja kutokana na mtu kuona amekulipa Milion moja,ukilipa Milion moja ni muda wa studio na Engineering ushanielewa’ – Majani.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni