burudan

https://share.bannersnack.com/bdtkqutzy/

26 Apr 2017

Ray C Foundation imewekwa pembeni – Ray C

Related image
Muimbaji Rehema Chalamila aka Ray C amedai taasisi yake ya kupambana na dawa za kulevya ‘Ray C Foundation’ ameamua kuiweka pembeni kwa muda ili afanye kwanza muziki.

Miaka miwili iliyopita muimbaji huyo aliianzisha foundation hiyo, kwaajili ya kuwasaidaia watu walioathirika na dawa za kulevya baada ya yeye mwenyewe kusaidiwa na aliyekuwa Rais wa wakati huo, Dk Jakaya Mrisho Kikwete.

Akizungumza na Bongo5 Jumanne hii kuhusu taasisi hiyo, Ray C amedai kwa sasa ameamua kujikita kwanza kwenye muziki ili kuijenga upya brand yake.

“Foundation kwa sasa nimeamua niiweke pembeni kidogo kwa sasa kwa sababu siwezi kushika mambo mawili kwa sasa. Sasa hivi nataka nguvu yangu kubwa niiweke kwenye kazi, kazi yangu ambayo iko kwenye damu kwa sababu muziki ni maisha yangu,” alisema Ray C.

Muimbaji huyo amedai mambo yake ya muziki yakikaa sawa ndipo atakaporudi kuanza kufanya vitu vingine.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni